• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mfuko wa Aga Khan watoa Ruzuku kwa Vikundi vya Wajasiriamali Mwanza

Posted on: June 30th, 2022


Mhe Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe Mhandisi Robert Gabriel ametoa rai kwa Vikundi vilivyofuzu kupata ruzuku kwa ajili ya kuendesha biashara katika kupambana na athari zitokanazo na ugonjwa wa Uviko 19 kuzingatia malengo ya mradi ili kufikia malengo.


Amesema hayo mapema leo kwenye Ukumbi wa Nyerere-Gold Crest Hotel wakati wa hafla ya Utoaji Ruzuku ya zaidi ya Tshs Milioni 169 kwa vikundi 90 vya huduma ndogo ya fedha iliyoratibiwa na Shirika la Aga Khan Foundation mradi unaolenga kupambana na athari za Ugonjwa wa Uviko 19 kwa jamii.


"Kipekee kabisa naomba nimshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia awamu ya Sita  ya uongozi wake kwa kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na nchi mbalimbali ikiwemo Umoja wa Ulaya ambao pia wamefadhili mradi huu wakishirikiana na Shirika la Aga Khan Foundation." Mkuu wa Mkoa.

"Hii ni fursa kubwa sana kwa mkoa kwa kupatiwa usaidizi wa kitaalamu na kifedha katika kuhakikisha wananchi wetu wanajengewa uwezo hivyo ni lazima mdhihirishe kwamba kule kuaminiwa kwenu kunaleta taswira kwamba Mwanza mradi ukileta unatekelezeka." Mhandisi Gabriel.

"Naomba niwasihi wanavikundi wote kuwa ruzuku hizi sio kwa ajili ya kufanyia sherehe au kujengea nyumba, mnapewa fedha kwa ajili ya kuendesha biashara zenu katika kujiinua kutoka kwenye umasikini." Simon Meigaro, Kaimu Mkurugenzi Mkazi The Aga Khan Foundation.

Mratibu wa mradi wa utoaji ruzuku kwa vikundi vya huduma ndogo ya fedha, Japhet Wange amesema vikundi vyote vilivyopo kwenye mradi huo vitapata ruzuku ya zaidi ya Milioni 169 na vinaanza rasmi kazi na kwamba mradi upo kwenye mfumo wa hisa ambazo zitaendeshwa kwa kutumia simu katika kufikia malengo.

"Mhe Mkuu wa Mkoa tuliandaa utaratibu wa kupata vikundi hivi na tunashukuru ofisi za Maafisa maendeleo za Halmashauri na Mkoa kwa usaidizi na hapa leo tupo na vikundi vya wawakilishi 90 ambavyo ndivyo vinaenda kupokea ruzuku hizi," amebainisha Wange.

"Vilevile, Mradi wetu unafanya kazi na vijana wajasiriamali na tunao vijana 100 kutoka kwenye mkoa huu ambao watajengewa uwezo wa kuboresha biashara zao ili waweze kujiinua na kuwaajiri hata vijana wenzao kwenye jamii." amefafanua.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.