• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MHANDISI LUHEMEJA: USAFI WA MAZINGIRA SASA NI LAZIMA KUTOKOMEZA MAGUGU MAJI

Posted on: March 10th, 2025

MHANDISI LUHEMEJA: USAFI WA MAZINGIRA SASA NI LAZIMA KUTOKOMEZA MAGUGU MAJI


Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhandisi Cyprian Luhemeja ametoa maagizo ya kufanyika kampeni maalum ya usafi wa mazingira kwenye mialo yote inayozinguka ziwa Victoria ili kutokomeza ukuaji wa magugu maji ambayo yamezidi kushamiri ziwani humo.

Akitoa maelekezo hayo mapema leo asubuhi Machi 10, 2025 kabla ya kuanza zoezi la kukagua hali halisi ya magugu maji hayo eneo la Kigongo Wilayani Misungwi, Luhemeja amebainisha kampeni hiyo ya usafi sasa siyo ya hiari bali ya lazima na kuwataka Wakurugenzi wote wa Halmashauri kuitikia wito huo ili kuepukana na hasara za kuwepo magugu maji hayo ziwani.

"Ndugu zangu hali halisi tunaiona mbele yetu siyo nzuri, hali ya usafiri inazidi kuwa ngumu na ukuaji wa viumbe maji upo hatarini, ni lazima hatua za haraka zianze tukianzia na azimio la usafi”. Amesisitiza Mhandisi Luhemeja.

Amesema wamelazimika kuja na Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe, Mwakilishi wa Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Maji, na Viongozi wengine waandamizi kutoka Tamisemi na Makatibu Tawala wa Mikoa kutoka Kanda ya ziwa, lengo ni kukutana na kutoa jawaba la haraka kulinusuru ziwa Victoria na janga hilo.

Aidha Katibu Mkuu huyo mara baada ya kupata taarifa fupi kutoka kwa Meneja wa Kanda wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira Bw. Joram Kayombo kwamba nchi ya Uganda wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutokomeza magugu maji, ameagiza wataalamu kutoka nchini kwenda huko ili kupata uzoefu wa kitaaluma ili kuja kusaidia kukabiliana na hali hiyo.

Awali akiwakaribisha Ofisini kwake viongozi hao waandamizi, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema magugu maji yamekuwa tishio katika kukuza uchumi wa buluu kutokana na uwepo wake kunashusha mazalia ya viumbe maji, shida ya usafiri na ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba nao kuwa mgumu.

"Nina imani na timu hii iliyochanganyika na wataalamu tofauti na masuala ya mazingira kuja na jawabu chanya ili kuendelea kulipa uhai ziwa Victoria”. Mhe. Mtanda.

Viongozi hao waandamizi kutoka Wizara mbalimbali siku ya kesho watakutana kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa le ngo la kutoa maazimio kukabiliana na janga hilo la magugu maji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.