• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MHE. MTANDA AWATAKA ASKARI WALIOFANYA VIZURI 2024 KUWA CHACHU KWA WENGINE 2025

Posted on: February 8th, 2025

MHE. MTANDA AWATAKA ASKARI WALIOFANYA VIZURI 2024 KUWA CHACHU KWA WENGINE 2025


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewapongeza Wakaguzi na Askari wote wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza waliotekeleza vizuri zaidi kwenye majukumu yao katika maeneo yao ya kazi hivyo kupelekea kupata vyeti vya Sifa na zawadi kwa mwaka 2024.

Mhe. Mtanda ametoa pongezi hizo leo Februari 08, 2025 alipokuwa akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Familia ya Polisi 2025 yaliyoadhimishwa katika viwanja vya FFU Mabatini, Jijini Mwanza na kuwataka Maafisa na Askari waliofanya vizuri kuwa chachu kwa wengine ambao hawakufanya vizuri.

Aidha RC Mtanda amewapongeza na kuwasihi kuendelea na ari na moyo huo wa kuchapa kazi kwa bidii, uaminifu, nidhamu na maarifa ya kupigiwa mfano, ujasiri, kujituma, kupenda kazi, kuwa na kauli nzuri na kutoa huduma nzuri inayozingatia haki kwa wananchi.

Kadhalika Mhe. Mtanda amesema Vyeti vya Sifa na zawadi zilizotolewa leo siku ya Familia ya Polisi ni kumbukumbu kwa sisi tuliopo na wanaokuja kwamba hawa Wakaguzi na Askari ni miongoni mwa Askari waliolifanyia vizuri zaidi katika jeshi la polisi na Wananchi kwa ujumla kwa mwaka 2024/2025.

“Ni matumaini yangu kuwa mafanikio yao yatakuwa kichocheo kwa Askari wengine ambao hawakupata vyeti vya Sifa na zawadi leo kuongeza bidii zaidi ili waweze kufikia na hata kuzidi viwango vya ubora wa kufanya kazi vizuri zaidi”.

Mhe. Mtanda pia amesema tunajivunia mchango mkubwa unaotolewa na Jeshi la Polisi katika kulinda usalama pamoja na maisha na mali za raia. Amesema anatambua kazi kubwa na nzuri waifanyayo iliyotufikisha hapa tulipo sasa.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Wilbrodi Mtafungwa amesema maadhimisho ya Siku ya Familia ya Polisi ni kiashiria cha kuwa mwaka mpya wa Kipolisi umefunguliwa rasmi amabapo wanashiriki pamoja kama familia kuadhimisha sherehe hiyo.

DCP Mtafungwa ameendelea kwa kusema kuwa zawadi zilizotolewa ni namna ya kutambua mchango na kazi nzuri iliyofanywa na Askari pamoja na Maafisa hao katika kutekeleza majuku ya jeshi la polisi la kulinda usalama wa raia na mali zao.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.