• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MIKOPO KWA WAFANYA BIASHARA WADOGO MWANZA IHARAKISHWE- WAZIRI GWAJIMA

Posted on: February 10th, 2025

MIKOPO KWA WAFANYA BIASHARA WADOGO MWANZA IHARAKISHWE- WAZIRI GWAJIMA


Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ametaka zoezi la utoaji wa mikopo kwa wafanyabiashara wadogo mkoani Mwanza lifanyike haraka kwani tayari Serikali imetoa fedha Tshs. bilioni 5.

Akizungumza leo Februari 10, 2025 kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza na viongozi wa Shirikisho la wafanyabiashara hao SHIUMA katika mkutano wa dharura, Waziri Gwajima ametoa maelekezo kuanzia ngazi ya Wizara yake,Mkoa na Halmashauri kuhakikisha mchakato wa awali wa usajili na hatimaye kupata vitambulisho ili wapate mikopo hiyo ukamilike haraka.

Awali kiongozi huyo mwandamizi wa Serikali mara baada ya kusomewa taarifa za usajili za wafanyabiashara hao kwenye Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza alionesha kutoridhishwa na idadi ndogo huku kasi ya usajili ikienda kwa kusua sua.

"Hii hali siwezi kuikubali licha ya kikao hiki cha dharura,nimewasikia watenda wote nilichokibaini ni baadhi kushindwa kutekeleza majukumu yao na mwishowe ni kuwachonganisha wafanyabiashara hao na Mhe.Rais,hii siyo sawa," Waziri Gwajima.

Kuhusu Mwanza kutopata Ofisi ya Shirikisho la SHIUMA, licha ya fedha kuletwa mkoani humo mara baada ya Rais kuridhia kutoa fedha kwa mikoa yote ya Tanzania Bara, amewataka viongozi hao kuandika barua kwa kufuata taratibu zote na nakala apatiwe ili aweze kupata nafasi ya kuijengea hoja suala lao na siyo kufanya mawasiliano kwa njia ya simu pekee.

Afisa Maendeleo ya Jamii mkoani Mwanza Bi.Janeth Shishila ameomba Wizara ione namna ya kuwawezesha vifaa zikiwemo Kompyuta maafisa maendeleo ngazi ya kata ambapo mchakato huo wa usajili unaanzia huko.

"Hali ya kusua sua usajili wa wafanyabiashara wadogo imechangiwa na watendaji kukosa vitendea kazi vya msingi na hakuna kifungu kinachowapa fedha huko kwenye halmashauri," amesisitiza Bi.Janeth.

"Tunamshukuru Rais kwa nia yake njema kwetu sisi wafanyabiashara wadogo lakini wapo baadhi wanao fanya hujuma ili hizi fedha zishindwe kuwafikia walengwa na kunufaika wasiohusika." Msemaji wa Shirikisho la wafanyabiashara, Jumanne Ayoub.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.