• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mkono wa pole wahanga MV nyerere waendelea kutolewa,zoezi la kuondoa meli majini,uopoaji miili

Posted on: September 25th, 2018


Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mwasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe amesema zoezi la uopoaji wa miili ambayo itakua imenasa na kugeuza kivuko na kukitoa majini bado linaendelea likiongozwa na jeshi la wananchi kwa kishirikiana na majeshi mengine.

“Mpaka kufikia jana meli ilikua imelala kifudifudi na sasa kimelala ubavu na Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo akiongoza zoezi hili,” alisema Kamwelwe.

Pia amewashukuru watanzania mbali mbali  walioguswa na wanaoendelea kuombea shighuli zinazoendelea Ukara.

Aidha zoezi la kupokea michango bado linaendelea ambapo wadau mbalimbali wanaendelea kujitokeza katika kichangia wananchi wa Ukara waliopatwa na Janga hili, miongoni mwa wadau walio wasilisha michango yao ni Baraza la maaskofu Jimbo la Dar es Salaam wameweka kwenye akaunti ya maafa kiasi cha shilingi Milioni 25. Na Benki ya KCB Tanzania Zuhura Muro nayo imetoa kiasi cha Shilingi Milioni 125 pesa imeshawekwa kwenye akaunti tayari. Nao Benki ya Shirika la Posta limeweka Milioni 10.

Kwa siku ya leo imepokelewa Milioni 160, Hivyo mpaka saa sita mchana fedha zilizochangwa zinafanya jumla ya shilingi  557,020,000/-

Mkuu wa Majeshi Tanzania Jenerali Venance Mabeyo amesema zoezi la kugeuza bado linaendelea vizuri na matumaini ya kugeuza kivuko ni mazuri mafundi na wataalamu wanaendelea kufunga Air Bags (maputo magumu yenye hewa) ili kisaidia kivuko kisimama. Na wakati zoezi hilo lilipokua linaendelea maiti moja ikapatikana. “Tunaendelea na kazi mpaka itakapo kamilika” Mabeyo.

Mtanzania mmoja anaitwa Abel Michael amewasilisha kiasi cha 100,000/- na mwenzake John Salia ametoa 200,000/-.

Katika hatua nyingine zoezi la kutambua miili linaendelea ambapo kuna familia moja iliyoweza kufika na kutambua ndugu yao aliyefariki miongoni mwa ile miili minne iliyokosa ndugu yao. Baada ya mahojiano ya masaa matano na ofisi za utambuzi wakaridhiwa kuwa yule aliyezikwa ni ndugu yao hivyo familia imeonyeshwa kaburi namba 8. Alisema Adam Malima Mkuu wa Mkoa wa Mara anaesimamia utambuzi wa miili katika kituo cha afya Bwisya katika kipindi hiki cha ajali.

Zoezi la Kulipa wafiwa na manusura wa ajali limeanza na fedha zinazotumika ni hii iliyochangwa na watanzani.

Michango inaendelea kutolewa wadau mbali mbali wanaendelea kutoa kama Kanisa la EAGT  waliotoa shilingi Milioni 5. Uwanja wa Ndege KIA Milioni 5, ATCL Milioni 10, River oil milioni 2, Olympic Oil milioni 10.

Jumla mpaka sasa ya fedha zote ni 589,320,000/=.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.