• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MKUU WA MKOA MWANZA AWASHUKURU KANISA LA AICT UWEKEZAJI SEKTA YA AFYA

Posted on: February 8th, 2025

MKUU WA MKOA MWANZA AWASHUKURU KANISA LA AICT UWEKEZAJI SEKTA YA AFYA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amelipongeza Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) kwa usimamizi na uendeshaji wa meli ya matibabu kwa kutoa huduma za afya

katika visiwa vya ziwa victoria kwa zaidi ya miaka 10.

Mhe. Mtanda ametoa pongezi hizo leo Februari 08, 2025 wakati wa Maadhimisho ya miaka kumi ya mpango wa meli ya matibabu ya MV Jubilee Hope Medical Ship na uzinduzi wa meli ya matibabu ya MV. Lady Jean yaliyofanyika katika viwanja vya Rock Beach Jijini Mwanza.

Mkuu wa Mkoa amewashukuru pia Washirika katika uendeshaji wa meli ya matibabu Vinetrust, (Geita Gold Mining Ltd – GGML), hivyo kufanikisha safari ya miaka 10 katika kutoa huduma za afya

katika visiwa vya ziwa victoria.

Sambamba na hilo ametoa shukrani za dhati kwa wadau wengine ambao ni Vine Trust UK kwa kushikiriana na Babcok kwa kufanikisha upatikanaji wa meli nyingine ya matibabu ambayo itasaidia kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma za afya kwenye Visiwa vya Ziwa Viktoria.

“Kwa kipindi cha miaka kumi, MV. Jubilee Hope imekuwa msaada mkubwa kwa jamii, ikitoa huduma za afya kwa maelfu ya watanzania waliopo visiwani ndani ya Ziwa Viktoria, ambako huduma za afya zilikuwa na changamoto katika upatikanaji wake”.

Kupitia huduma hizi, tumeshuhudia mafanikio makubwa katika kupunguza magonjwa, kuokoa maisha, na kuboresha ustawi wa jamii kwa ujumla. Ameongeza Mhe. Mtanda.

Kadhalika Mkuu wa Mkoa amesema Uzinduzi wa MV. Lady Jean ni Hatua Mpya ya Maendeleo katika kuendeleza huduma za matibabu kwa wakazi wa Ziwa Viktoria.

Ambapo Meli hiyo mpya itaimarisha juhudi za huduma za afya kwa jamii ya visiwani kwa Kupanua wigo wa utoaji wa huduma za matibabu kwa idadi kubwa zaidi ya wagonjwa 7, Kuboresha utoaji wa huduma za dharura kwa haraka na kwa ufanisi mkubwa zaidi.

“Hivyo, tunawashukuru sana kanisa la AICT kwa kuja na mradi wa Afya kupitia meli hii ya Matibabu ya MV. Lady Jean”.

Naye Askofu wa Kanisa la AICT Mussa Magwesela, amesema anaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushirikiano wanaoupata kuanzia walipoanza rasmi shughuli za utoaji wa matibabu kwa njia ya Meli ambapo kwa takribani miaka 10 sasa tangu pale walipoanza rasmi mnamo mwaka 2015

Kadhalika amesema Kwa miaka kumi iliyopita, wanajivunia mafanikio kama vile Huduma za afya zimetolewa kwa zaidi ya watu 500,000 katika visiwa vya ziwa Viktoria kwenye utoaji wa chanjo, matibabu ya malaria, huduma za afya ya uzazi, upasuaji mdogo na huduma za afya ya kinywa na meno.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.