• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mradi wa kurejesha Ardhi iliyoharibika wasaidia kuondoa uhaba wa chakula Magu

Posted on: September 1st, 2023

Mradi wa kurejesha Ardhi iliyoharibika wasaidia kuondoa uhaba wa chakula Magu


Wananchi Wilayani Magu wamelishukuru Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD) kwa kuwaletea miradi inayosaidia kurejesha Ardhi iliyoharibika ambapo wamesema  imewahakikishia upatikanaji wa chakula cha kutosha na usalama wa chakula kwenye kaya zao.

Hayo yamebainika leo kwenye kijiji cha Lumeji kata ya Sukuma-Magu wakati wa ziara ya Makamu Rais wa shirika hilo alipotembelea mradi wa ufugaji Kondoo ambapo wananchi wamebainisha kuwa mradi huo umewasaidia pamoja na kuuza Kondoo kutokana na kuzaliana vilevile unawapatia mbolea ya asili wanayoitumia kwenye kilimo na kuongeza uzalishaji.

Akizungumza kwa niaba ya kikundi cha ufugaji Kondoo Ndugu Ernest Pamba amesema awali kwenye eneo lao walikua wanakumbwa na changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi lakini kupitia mradi huo wameweza kuuza kondoo na kupata mbolea ya asili wanayoitumia kwenye mashamba.

Vilevile, ametoa wito kwa Serikali kendelea kuleta miradi yenye tija kama hiyo na kuboresha kwa kuipanua kwenye maeneo mengi ili wananchi walio wengi wapate kujifunza teknolojia na kuboresha hali ya usalama wa chakula na kuhakikisha upatikanaji wa chakula cha kutosha.

Makamu Rais wa Shirika hilo Donal Brown

amesema amefurahishwa na utekelezaji mzuri wa miradi wilayani humo na ameahidi katika wakati mwingine wataangalia namna ya kuboresha kama vile kuwaletea miradi ya mabwawa ya maji  ili kukabiliana na ukame.

"Nawapongeza kwa mradi mzuri wa ufugaji kondoo mmeufanya vizuri nami hii ndio taaluma yangu, nimegundua kuwa tatizo kubwa hapa ni maji katika uboreshaji wa miradi yetu baadae tutaangalia namna ya kuleta mabwawa."

Bwana Brown.

Naibu Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Sweetbert Mkama ametoa wito kwa wananchi kutunza miradi hiyo huku akibainisha kuwa itawasaidia kwenye nyanja mbalimbali za chakula na uhifadhi wa mazingira na vilevile ametumia wasaa huo kuwaomba IFAD kuleta miradi mingine kwa ajili ya kusaidia jamii hiyo kwani mahitaji ni makubwa bado.

Emil Kasagara aliyemwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita kwa kuweka mazingira wezeshi ya wahisani kuja kusaidia wananchi na amefafanua kuwa mbolea inayopatikana kwenye mradi wa ufugaji kondoo inasaidia kuzalisha mazao na kuimarisha usalama wa chakula.

"Nchi kumi na mbili barani Afrika zinafadhiliwa na miradi mbalimbali ya uhifadhi wa mazingira, lakini mradi huu unaogharimu zaidi ya Bilioni 1 wilayani Magu umejikita kwenye sekta za ufugaji, kilimo na umwagiliaji na una lengo la kuimarisha upatikanaji wa chakula, kutunza mazingira na kuondoa utapiamlo. Amesema Joseph Kihaule mratibu wa miradi ya GEF IFAD- LDFS nchini.

Naye, Tabu Daudi mwanakikundi katika Shamba darasa la Mihogo Nyang'hanga amebainisha kuwa mradi huo umesaidia kuwapatia chakula cha kutosha kwani mbegu hiyo (TZ 130) inakomaa ndani ya miezi tisa tu tofauti na mbegu za asili walizokua wanalima siku za nyuma.

"Tulikua na mbegu ambazo zilikua ngumu kukomaa ila sasa kwa mbegu hii ya kisasa imetupa chakula cha kutosha na hata kuweza kuuza kingine na kupata fedha za kujikimu, kwakweli hii mbegu imefukuza njaa na tunawashukuru sana maafisa Ugani kwa kutuongoza vizuri", amesisitiza.

Masalu Issa amesema amefanikiwa kulima shamba la Viazi kutokana na uwepo mradi wa umwagiliaji na kwamba yupo kwenye mpango wa kulima Viazi lishe kwani shirika hilo limeleta maji ya kutosha kuhudumia mashamba yao naye ana malengo ya uzalishaji mkubwa zaidi kwenye siku za usoni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.