• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MRADI WA UMWAGILIAJI IBANDA–IGAKA WA BILIONI 35 HAUTASIMAMA – SILINDE

Posted on: January 10th, 2026

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. David Silinde amesema mradi wa umwagiliaji wa Ibanda–Igaka unaotekelezwa katika Mikoa ya Geita na Mwanza utaendelea kutekelezwa kama ulivyopangwa licha ya kuwepo kwa changamoto ya madai ya fidia kutoka kwa baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Sengerema, Mkoa wa Mwanza.

Mhe. Silinde ametoa kauli hiyo Januari 10, 2025 wakati wa kikao kifupi na Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana aliyewasilisha taarifa ya sintofahamu iliyojitokeza kuhusu fidia kwa wananchi wanaotakiwa kupisha maeneo yao kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.

Naibu Waziri amesema Wizara ya Kilimo haina fungu la moja kwa moja la kulipa fidia lakini serikali itaendelea kutumia njia ya elimu, mazungumzo na uhamasishaji kwa wananchi ili waelewe umuhimu wa mradi huo katika kuongeza uzalishaji wa kilimo, usalama wa chakula na ajira.

“Mradi hautasimama. Tutatumia elimu na njia nyingine za mazungumzo ili kuhakikisha utekelezaji unaendelea,” amesema Mhe. Silinde.

Akizungumza katika kikao hicho Bw. Balandya alisema sekta ya kilimo ni miongoni mwa sekta muhimu zinazochangia uchumi na kuajiri watu wengi, hivyo kuna umuhimu wa kuhakikisha kilimo kinafanyika kwa tija kupitia umwagiliaji.

Amesema Mkoa wa Mwanza umebarikiwa kuzungukwa na Ziwa Victoria jambo linalotoa fursa kubwa ya kuendeleza kilimo cha umwagiliaji badala ya kutegemea mvua, sambamba na kusaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.

“Tuna vijana wengi hapa Mwanza wasio na ajira. Tunategemea kilimo hususani cha umwagiliaji kiwe suluhisho la changamoto hiyo”.

Bw. Elikana amezihimiza Halmashauri kuweka mazingira wezeshi kwa shughuli za kilimo na mifugo kwa kutumia fedha za maendeleo kujenga miundombinu muhimu kama maeneo ya umwagiliaji, majosho ya mifugo na kutenga maeneo maalum kwa vijana kujihusisha na kilimo na ufugaji.

Ameeleza kuwa ingawa matumizi ya fedha za maendeleo kwa sasa yana masharti, bado kuna fursa ya kuzitumia kujenga miundombinu itakayochochea ajira na maendeleo kwa vijana.

Mradi wa Ibanda–Igaka, unaogharimu takribani Shilingi bilioni 35, upo mpakani mwa Wilaya ya Sengerema (Mwanza) na Mkoa wa Geita.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA UMWAGILIAJI IBANDA–IGAKA WA BILIONI 35 HAUTASIMAMA – SILINDE

    January 10, 2026
  • RC MTANDA MGENI RASMI MECHI YA KIRAFIKI SIMBA VS PAMBA MWANZA

    January 10, 2026
  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.