• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MTANDA ATETA NA WATUMISHI KWIMBA, ATAKA NIDHAMU KAZINI ILI KUWALETEA MAENDELEO WANANCHI

Posted on: June 6th, 2024

RC MTANDA ATETA NA WATUMISHI KWIMBA, ATAKA NIDHAMU KAZINI ILI KUWALETEA MAENDELEO WANANCHI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Juni 06, 2024 amezungumza na watumishi wa Halmashauri na Wilaya ya Kwimba Kwimba na akatumia wasaa huo kutoa dira ya kuwaletea wananchi maendeleo kupitia majikumu yao kuwa ni uzingatiaji wa nidhamu katika kazi.

Akizungumza na watumishi hao kwenye Ukumbi wa Halmashauri, Mtanda amewataka watumishi hao kuacha kuishi kwa mazoea na badala yake wawe na nidhamu ya kuwahi kazini na kujituma ili kuhakikisha wanawatumikia wananchi kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za miongozo.

Aidha, amewataka amewataka watumishi kujenga umoja baina ya taasisi moja na ingine ndani ya wilaya na kushirikiana kwenye kazi na kuepuka tabia ya ubishani au makundi kazini ili kila mmoja ajue ana wajibu wa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria na sio kwa ajili ya mtu fulani na vinginevyo.

Vilevile, amewapongeza kwa ukusanyaji wa Mapato hadi kufikisha shilingi Bilioni 3.5 kutoka Bilioni 2 za siku za nyuma na amewakumbusha kutumia fedha kwa mujibu wa Miongozo iliyopo kwa kutenga 10% za Makundi ya kisheria, 40% za miradi ya maendeleo na kuhakikisha wanaweka fedha benki.

Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija amesema kuwa upatikanaji wa Maji vijijini kwa sasa ni asilimia 62 na ipo miradi kadhaa ya maji inaendelea kutekelezwa na kwamba itakapokamilika itasaidia wilaya hiyo kufikia asilimia zaidi ya 70 ya upatikanaji maji safi.

Aidha, amebainisha uwepo wa nishati ya umeme kwenye vijiji vyote wilayani huku akifafanua kuwa ukusanyaji wa mapato kupitia TRA wamekusanya zaidi ya Bilioni 2 tofauti na Bilioni 1 waliyoikusanya mwaka uliopita ikiwa ni ongezeko linalotokana na sera nzuri za serikali ya awamu ya sita.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.