• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MUITIKIO MDOGO WA WANAFUNZI KURIPOTI SHULENI, RC MTANDA ATOA MAAGIZO

Posted on: January 20th, 2026

Halmashauri ya Wilaya Sengerema imepokea Tshs. Bilioni 2.16 katika mwaka wa fedha 2025/26 kwa ajili ya kujenga miradi 9 ya elimu zikiwemo shule mpya 4 fedha zilizokusudiwa kupunguza msongamano darasani na kuwapunguzia wanafunzi umbali wa kufuata elimu.

Akikagua miradi ya Elimu leo tarehe 20 Januari 2026 wilayani humo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka viongozi na watendaji wa halmashauri hiyo kuhamasisha wazazi na walezi wanawapeleka watoto shule katika ngazi zote kuanzia awali, msingi na kidato cha kwanza.

Mhe. Mtanda amewataka watendaji kuhakikisha wanapita nyumba kwa nyumba kuzungumza na wazazi na ili wawapeleke watoto shuleni huku akitolea mfano wa wanafunzi wa kidato cha kwanza kuwa ni asilimia 19 pekee (1561) ya walioandikishwa (7987) ndio wameripoti mpaka sasa.

Ameongeza kuwa wazazi wahamasishwe kuchangia mpango wa chakula shuleni ili wanafunzi wawe na nguvu ya kusoma na kupokea wanachofundishwa kwani wana uhakika wa chakula kilichozingatia lishe bora wakati wa masomo.

“Chakula kwa wanafunzi ni wajibu wa wazazi, hatuwezi kuwa na maendeleo mazuri kitaaluma ikiwa watoto wanashinda njaa shuleni hivyo twendeni tukahamasishe wazazi watoe michango halali iliyoidhinishwa na mamlaka.” Amesema Mhe. Mtanda

Akizungumza katika nyakati tofauti wakati akakikagua ujenzi wa shule mpya za Msingi Sima na Tabasamu Mhe. Mtanda ameagiza kasi ili kufanya ukamilishwaji wa haraka wa miradi yote hadi kufikia februari 28, 2026 ili wanafunzi wapate elimu katika miundombinu kamili.

Aidha, amewataka Wakala ya Maji vijijini (RUWASA) kuhakikisha wanapeleka huduma ya maji kwenye Taasisi na kwa wananchi wa Kata ya Sima kwani tayari serikali imejenga mradi mkubwa wa maji na kwa TARURA amewataka kurekebisha barabara ya kwenda kwenye shule mpya ya Tabasamu.

Akizungumza na wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha sita katika shule ya sekondari Mtunduru Mhe. Mtanda amewataka kusoma kwa bidii na kuacha kujihusisha na mapenzi wawapo shuleni na wazazi kuhakikisha wanawapa nafasi watoto wa kike kupata elimu kama wanavyopata wa kiume.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MTAKUWAA MWANZA YAWEZESHA KUPUNGUZA WATOTO WA MTAANI KWA 50%

    January 26, 2026
  • RC MTANDA: DHAMIRA NI MSINGI WA KUFANIKISHA SHUGHULI ZA MWENGE WA UHURU 2026

    January 26, 2026
  • NDC WAHITIMISHA ZIARA YA MAFUNZO MWANZA

    January 23, 2026
  • WAZIRI MKUU AZINDUA MELI MPYA YA MV NEW MWANZA, ATOA MAAGIZO KWA MIRADI ILIYOSIMAMA

    January 23, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.