• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWANZA WAONGOZA MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU KANDA YA ZIWA

Posted on: August 20th, 2024

MWANZA WAONGOZA MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU KANDA YA ZIWA


Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Emily Kasagara leo Agosti 20, 2024 ametangaza matokeo ya utamilifu kidato cha nne kwa mikoa ya kanda ya ziwa ya Geita, Simiyu, Kagera, Mara na Mwanza yenye ufaulu wa GPA 3.9 kwa asilimia 84.48 (Daraja la kwanza hadi la nne).

Akitangaza matokeo hayo Kasagara amefafanua kuwa ufaulu wenye tija daraja I- III ni asilimia 26.48 GPA ya 2.4 na kwamba ufaulu umejikita katika daraja la 4 kwa asilimia 13.01 huku daraja sifuri ni asilimia 9.02 na akawataka walimu kuwajibika ili kupandisha ufaulu hususani madaraja 1, 2 na 3.

"Mkoa wa Mwanza umeongoza kwa GPA ya 3.72 kwa asilimia ya ufaulu wa asilimia 86.13 ikifuatiwa na Mkoa wa Simiyu na tunazipongeza halmashauri za Manispaa ya Ilemela, Jili la Mwanza na Bukombe DC kwa kufanya vizuri." Amesema Kasagara.

Vilevile, ndugu Kasagara ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kuamini kuwa elimu ndio nyenzo ya kuaminika inayowezesha kila mtu kuyakabili mazingira yake kwa usahihi kwa kujipatia maendeleo endelevu kwa kutoa fedha za elimu bila ada kwa shule za msingi na sekondari jambo linalochangia kukuza ufaulu.

"Serikali imeendelea kuimarisha miundombinu kwa kukarabati shule kongwe na kujenga shule mpya na kuongeza miundombinu kama madarasa, mabweni, maabara na vyoo." Ameongeza Kasagara.

Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza Martin Nkwabi amefafanua kuwa malengo ya mitihani hiyo siyo kujikita tu kwenye kuona mwanafunzi amefeli au amefaulu bali ni kujipima kwenye ufundishaji wa walimu ili kurekebisha kasoro kwa ajili ya kufanya vizuri kwenye mitihani wa mwisho ya kumaliza elimu ya sekondari.

Aidha, amewataka walimu kuwajibika kuhakikisha wanapandisha matokeo kwa watoto kwenye madaraja ya kwanza hadi la tatu kama walivyowekeana malengo hususani mkoa wa Mwanza ili kuhakikisha wanafuta daraja ziro na kupunguza daraja la nne kwa wanafunzi.

"Nataka kila mkuu wa shule afanye tathmini na akatafute sababu ya matokeo aliyoyapata na kuhakikisha anarekebisha kasoro hizo ili tupate ufaulu wa zaidi ya asilimia 60 kwa wanafunzi wetu ili kuhakikisha tunafuta daraja ziro na daraja la nne." Afisa Elimu Mkoa.

Matokeo hayo ya mtihani uliofanyika  Julai mwaka huu yanapatikana kupitia https://sras.ac.tz ambapo kila mmoja anaweza kuona na yamepangwa kwa mpangilio wa mikoa, halmashauri na shule.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.