• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza Yazindua Kampeni ya Uzazi Salama

Posted on: April 2nd, 2019

Wizara ya Afya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Afya na Ustawi wa Jamii Mkoani Mwanza wamezindua Kampeni   ya Uzazi Salama ijulikanayo kama "Jiongeze Tuwavushe Salama".

Kampeni hiyo imezinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella ikiwa na kauli mbiu ya "Kila mmoja wetu anao wajibu wa kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi.Maneno basi, sasa vitendo."

Akiongea katika uzinduzi huo Mhe.Mongella amesema vifo hivyo vinaepukika hivyo jamii ina jukumu kwa kuhakikisha inatambua dalili hatarishi na kuwasaidia wazazi na watoto wachanga.

"Katika kuhakikisha kuwa Vifo hivi vinapungua Serikali ya awamu ya  tano ya Mhe. Dkt.John Magufuli imejenga vituo vya afya 352 Nchi nzima na kuongeza upatikanaji wa dawa ili kusaidia wazazi na kiwavusha salama," aliaema Mongella.

Naye Katibu Tawala Msaidizi kwa upande wa Afya Dkt.Thomas Rutachunzibwa amesema kampeni hii  ina maana kuwa viongozi mbalimbali wakitumika  ipasavyo watachangia kumvusha mzazi salama na haipaswi kuachiwa wadau wa afya pekee.

"Swala la vifo bado ni tatizo tusiwaachie wadau wa afya pekee tubadirishe mtazamo kuhusiana na vifo vya wazazi na watoto wachanga kila mdau ana wajibu wa kumvusha mzazi  salama,"  alisema Dkt. Rutachunzibwa.

Aidha Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Christopher Kadio amesisitiza kuhusu Afya ya uzazi na kumtaka kila kiongozi kuwajibika katika kufanikisha Kampeni hii ya kumvusha mzazi  salama, hii inaweza kufanyika katika ngazi mbalimbali katika maeneo yetu ya kazi.

"Sisi tuliopo humu ndani tujiulize, umefanya nini katika kupunguza vifo vya wazazi na watoto wachanga hasa katika maeneo tuliyopo?" Alisema Kadio.


Mkoa wa Mwanza ni Mkoa wa nne kutekeleza uzinduzi wa kampeni hii ambayo Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan aliizindua Kitaifa mwaka 2018 kwa lengo la kutokomeza kabisa vifo vya akina mama na watoto wachanga kwa kujiongeza na kuwavusha salama.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.