• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza Yazindua soko la Madini

Posted on: May 8th, 2019



Waziri wa Madini, Doto Biteko amesema, katika kuhakikisha kwamba mchango wa sekta ya madini unaifikisha nchi kwenye uchumi wa kati ifikapo 2025, masoko ya madini ni muhimu.

Ameyasema hayo leo, alipokuwa akizindua soko la madini la Mkoa wa Mwanza ambapo amewataka viongozi mbalimbali wa serikali katika ngazi zote kushiriki kikamilifu katika kutekeleza mipango iliyowekwa na Serikali kupitia Wizara yake ili kuifikisha nchi katika uchumi huo wa kati.

Biteko amesema, wizara imechukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kikao cha Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu

Tawala wa Mikoa kilichofanyika mwezi Januari, 2019 Jijini Dodoma kikao kilicholenga kujenga uelewa wa pamoja juu ya maudhui ya kanuni wa uanzishwaji masoko ya madini nchini.


Aliendelea kusema, katika kuelekea uanzishwaji wa masoko ya madini nchini ulioanza mapema mwezi Februari, wizara ilifanikiwa kufanya mafunzo kwa Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi pamoja na Makatibu Tawala wa Wilaya.

Pamoja na jitihada hizo, Wizara ilifanikiwa kufanya Mkutano Mkubwa wa kisekta mwishoni mwa mwezi Januari 2019 na kupokea  maoni mbalimbali ya wadau yaliyopelekea Serikali kufanya mabadiliko ya sheria ya mwaka 2019 iliyohusisha utungwaji wa kanuni za masoko kwa ajili ya kuanzishwa masoko ya madini.


Aidha, Biteko amesema serikali ilikubali ombi la wadau la kupunguza utitiri wa kodi na tozo mbalimbali kwa wachimbaji wadogo na kuamua kufuta baadhi ya kodi hizo ikiwemo kodi ya zuio (withholding tax) pamoja na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwa wachimbaji wadogo.

Akizungumzia historia ya uanzishwaji wa soko la madini mkoani Mwanza, Biteko alisema ilianza mnamo mwaka 2018 wakati wizara ilipounda kamati maalum kwa lengo la kubaini sababu ya utoroshwaji wa madini hasa madini ya dhahabu na vito.


Biteko anasema pamoja na hilo kamati ilibaini kuwa utitiri wa kodi na tozo mbalimbali zilizokuwa zikitozwa kwa wachimbaji wadogo wa madini ni sababu nyingine iliyochangia utoroshwaji wa madini nchini na kukiri chimbuko la uanzishwaji wa masoko ya madini kuwa ni Mwanza kupitia kamati hiyo.


“Uzinduzi wa soko hili unatoa majibu kwa maswali ya wananchikuhusu changamoto ya utoroshwaji wa rasilimali madini ambayo imedumu kwa muda mrefu” Biteko alikazia.


Aidha, Biteko amewataka wadau wote katika mnyororo mzima wa uendeshaji wa masoko ya madini kutimiza wajibu wao kwa uzalendo wa kiwango kinachostahili.


Kwa upande wake katibu Mkuu wa Madini, Prof. Simon Msanjila amewataka viongozi wa serikali kushiriki kikamilifu katika kusimamia rasilimali madini inayopatikana nchini.

Akielezea idadi ya masoko yaliyofunguliwa mpaka sasa, Prof. Msanjila alisema ni masoko ya madini 13 na siku ya leo masoko ya madini manne yanafunguliwa likiwemo la Mwanza, Kagera, Iringa na Songwe wakati taratibu za kukamilisha zoezi hilo kwa mikoa iliyosalia nchi nzima zikiendelea.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella alisema, Mkoa wa Mwanza unazalisha madini ya dhahabu na madini ya ujenzi kwa kiasi kikubwa katika wilaya ya Kwimba na Misungwi na kiasi kidogo katika maeneo ya Sengerema. Alikiri uwepo wa uzalishaji wa madini ya almasi kwa kiwango kidogo katika maeneo ya Mabuki na Manangwa wilayani Misungwi.

Mongella amebainisha kuwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza wana imani kuwa usimamizi mzuri wa sekta ya madini utaipelekea nchi kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.