• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAIS SAMIA AZINDUA MRADI WA MAJI BUTIMBA, ALETA KICHEKO KWA WANA MWANZA

Posted on: June 20th, 2025

RAIS SAMIA AZINDUA MRADI WA MAJI BUTIMBA, ALETA KICHEKO KWA WANA MWANZA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan leo juni 20, 2025 amezindua mradi wa Maji na chanzo cha kutibu na kusafisha maji uliojengwa na Kampuni ya Sogea Satom na Vinci Grand Projects kutoka Ufaransa kwa thamani ya zaidi ya Tshs. Bilioni 70.


Akizungumza na wananchi katika hafla ya iliyofanyika katika viwanja vya mradi huo Butimba jijini Mwanza Mhe. Rais amesema mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha lita milioni 48 kwa siku utasaidia kuongeza mtandao wa usambazaji maji ndani na maeneo ya pembeni mwa jiji hilo takribani watu 450,000.


Aidha, amewapongeza MWAUWASA kwa usimamizi na amewashukuru wadau wa maendeleo waliotoa ruzuku na mikopo pamoja na Mkandarasi kwa ujenzi wa mradi huo na akawataka wananchi kulinda miundombinu ya mradi huo kwa manufaa ya vizazi vya sasa na baadaye.


Ameongeza kuwa miradi ya maji na usafi wa mazingira inayotekelezwa kila kona nchini imedhamiria kutegua kitendawili cha upatikanaji wa maji safi na salama na akawasihi wananchi kujenga uchumi wao kwa uvuvi na kilimo lakini wahakikishe wanahifadhi mazingira na vyanzo vya maji.


Naye, Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amebainisha kuwa awali mkoani wa Mwanza ulikua na chanzo kimoja tu kikubwa cha maji cha Capripoint ambacho kinazalisha lita milioni 90 kwa siku na kwamba kutokana na ongezeko la watu chanzo hicho kimekua finyu na ndipo serikali ikaamua kujenga chanzo kipya.


“Mhe. Rais, ilikuwa ni kitendawili kikubwa, wana mwanza wa Nyamagana na Ilemela walikuwa wanahoji kwanini ziwa lipo mwanza na wao wanakosa maji”, amesema Mhe. Aweso.

Mkuu wa Mkoa Mhe. Said Mtanda amesema mahitaji ya maji kwa sasa ni lita milioni 172 kwa siku huku vyanzo vya Capripoint na Butimba vikizalisha lita 138 na kwamba vimesaidia kuongeza kiwango  cha upatikanaji Maji kutoka 59% (2021) hadi 85% (2025) sawa na ongezeko la asilimia 25.


Aidha, amefafanua kuwa sekta ya maji Mkoani Mwanza imeimarika sana kwani kwa vijijini kupitia Wakala ya Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wametekeleza miradi zaidi ya 180 yenye thamani ya zaidi Bolioni 100.3 na hali ya upatikanaji imeongezeka hadi zaidi ya asilimia 78.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMA TUNAHITAJI KUSONGA MBELE NI LAZIMA KUJIUNGA NA USHIRIKA – RAS BALANDYA

    June 24, 2025
  • RAS BALANDYA AFUNGUA MAFUNZO YA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA

    June 23, 2025
  • SHEREHE ZA BULABO KUPANDISHWA HADHI KUWA URITHI WA UTAMADUNI

    June 21, 2025
  • SUNGUSUNGU DAY YAFANA MWANZA, RAIS SAMIA ASIMIKWA UTEMI

    June 20, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.