RAS BALANDYA AFUNGUA MAFUNZO YA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana leo terehe 23 juni, 2025 amefungua rasmi mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa Kielektroniki wa Usimamizi wa Utendaji kwa Watumishi wa Umma ( PEPMIS) yenye lengo la kuwajengea uwezo watumishi wa umma katika matumizi sahihi ya mfumo huo.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Ndugu Balandya amesema mafunzo yatawajengea uwezo watumishi wa Umma ili waweze kutoa Taarifa ya utekelezaji na kupimwa majukumu yao kupitia mfumo wa usimamizi wa utendaji kazi wa Utumishi wa Umma.
“Ni matarajio yangu kuwa mafunzo haya yatatusaidia kuongeza uelewa na umakini kuhusu mfumo unavyofanya kazi na kuboresha uwajibikaji kwa kila mtumishi”.
Ninaamini mtatumia vyema fursa ya mafunzo haya na yataenda kuimarisha uelewa wa mfumo Ili muwe na uwezo mkubwa wa kupanga majukumu yenu. Ameongeza Katibu Tawala.
Kadhalika, Ameeleza ametumia wasaa huo kueleza umuhimu wa kufanya kazi kwa bidii kwa kuwataka watumishi wa umma kufanya kazi kwa kujituma na kujitoa kwa moyo Ili kuweza kufikia malengo.
Mafunzo hayo yameratibiwa na wakufunzi kutoka Ofisi ya Rais – Menejiment ya Utumishi wa Utawala Bora ambayo yamehusisha washiriki kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, wakiwemo Wakuu wa Sehemu na Vitengo, Wakurugenzi wa Halmahsauri, Makatibu Tawala wa Wilaya, pamoja na watumishi kutoka taasisi mbalimbali.
Kwa upande wao, washiriki wa mafunzo hayo wameeleza kuwa yamewasaidia kupata uelewa wa kina kuhusu mfumo huo na umuhimu wake katika kuboresha uwajibikaji na utendaji kazi wa kila mtumishi.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.