• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA ATOA MAAGIZO KWA BARAZA LA MADIWANI UKEREWE USIMAMIZI WA HALMASHAURI

Posted on: June 17th, 2025

RAS BALANDYA ATOA MAAGIZO KWA BARAZA LA MADIWANI UKEREWE USIMAMIZI WA HALMASHAURI


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana ametoa maagizo kadhaa kwa baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ikiwemo kusimamia Halmashauri hiyo kwa uzalendo ili kuwasaidia wananchi hususan kwenye matumizi ya fedha za umma.

Ametoa maagizo hayo mapema leo juni 17, 2025 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa katika Baraza Maalum la kupitia hoja na taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali kwa halmashauri ya wilaya hiyo kwa mwaka 2023/24 lililofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo mjini Nansio.

Aidha, Ndugu Balandya ameitaka Halmashauri hiyo kuendelea kujibu hoja za Mkaguzi na kuendelea kushirikiana na Ofisi hiyo kwa kuwa Halmashauri inaye Mkaguzi wa ndani hivyo amewataka kumtumia Mkaguzi huyo ili aisaidie Halmashauri kuweza kujifahamu hali zao kabla Mkaguzi wa nje hajafika.

Kuhusu hoja ya utumiaji usioridhisha wa mfumo wa usimamizi wa mali za serikali (GAMIS), Katibu Tawala ameagiza halmashauri hiyo ndani ya kipindi cha robo ya kwanza kutumia wataalamu kutoka Sekretarieti ya Mkoa kuwajengea uwezo wataalam wa ugavi ndani ya halmashauri hiyo ili kumaliza tatizo.

Mkuu wa wilaya hiyo Mhe. Christopher Ndubiagai ametumia baraza hilo kuwakumbusha wajumbe wa baraza hilo kusimamia makusanyo na matumizi ya fedha za umma kwa masilahi ya wananchi wa Ukerewe na akawaalika kushiriki ziara ya Mhe. Rais atakayoifanya juni 19-21 Mkoani humo.

Kaimu Mkaguzi Mkuu wa Nje Mkoa wa Mwanza ndugu Henry Chausa amebainisha kuwa kwa mwaka wa 2023/24 halmashauri ya wilaya ya Ukerewe ilifanyiwa ukaguzi kwa hesabu na kupata hati inayoridhisha na kwa miaka mitatu mfululizo imeendelea kupata hati inayoridhisha.

"Hoja za miaka ya nyuma halmashauri ilikua na mapendekezo 18 na baada ya uhakiki 16 zipo kwenye hatua za utekelezaji na 2 bado hazijafanyiwa kazi pamoja na agizo 1 la LAAC kutokana na kukosekana na kukosa vielelezo na mkakati wa CMT kujibu hoja." Amesema Chausa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS BALANDYA ATAKA MIRADI YA MAENDELEO KUKAMILIKA KWA WAKATI

    June 17, 2025
  • RC MTANDA AAGIZA HOJA ZA KIMAKOSA KUMALIZWA HARAKA

    June 17, 2025
  • RC MTANDA ATOA MIEZI 2 KWA MANISPAA ILEMELA KUTENGENEZA MAGARI YASIYOTEMBEA

    June 17, 2025
  • RAS BALANDYA ATAKA MIKAKATI KUINUA UFAULU WA WANAFUNZI MAGU

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.