• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS MWANZA AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA FEDHA KUSIMAMIA MPANGO WA M-MAMA

Posted on: August 17th, 2024

RAS MWANZA AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA FEDHA KUSIMAMIA MPANGO WA M-MAMA


Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Daniel Machunda amezitaka Halmashauri zote za Mkoa huo kutenga bajeti za kutekeleza mpango wa M-Mama unaotekeleza rufaa kwa ajili ya matibabu kwa wajawazito, waliojifungua na watoto ili kukomesha vifo vitonanavyo na uzazi.

Bwana Machunda ametoa wito huo mapema leo Agosti 17, 2024 wakati akifungua kikao kazi cha kujadili uendelevu wa mfumo wa usafirishaji wa wajawazito, waliojifungua na watoto kwenda kupata huduma za afya M- Mama katika hoteli ya Adden Palace Ilemela.

Aidha, ameagiza vituo vya afya kuweka mikakati thabiti ya upokeaji wa rufaa na  waratibu wa zoezi hilo kusimamia kwa weledi na wakati ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya wakati wote na kuhakikisha Taifa linakua na uzazi salama wakati wote.

"Vifo vitokanavyo na uzazi vinaumiza sana, ni lazima tuhakikishe kujifungua kunakua ni neema na sio janga kwa jamii kwani ni jambo la neema tulilopewa na Mwenyezi Mungu", amesisitiza ndugu Machunda ambaye ni Katibu Tawala Msaidi sehemu ya Utawala na Usimamizi wa rasilimali watu.

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Jesca Lebba amesema mfumo wa usafirishaji wa dharula kwa wajawazito, waliojifungua pamoja na watoto una miezi 18 tangu kutambulishwa Mwanza na rufaa zilianza kwa kupiga namba 115 na kwamba Serikali imeshirikiana na wadau wakati wote kufanikisha rufaa.

Aidha, amesema pamoja na majukumu mengine waratibu wamekagua na kuweka vifaa kwenye uratibu wa kituo cha kupokelea wagonjwa cha hospitali ya rufaa ya Mkoa Sekou Toure na kwamba rufaa 4775 zimefanyika na Jumla ya Milioni 14.4 zimechangwa kwenye akaunti ya Taifa.

Meneja wa kanda wa shirika la Pathfinder Charles Kato amesema kuwa wanayo furaha kukabidhi majukumu ya utekelezaji wa usafiri wa dharula kwa wajawazito, waliojifungua pamoja na watoto na kwamba wataendelea kushirikiana na Serikali katika kushauri masuala mbalimbali.

Vilevile, Meneja huyo amebainisha kwamba wahisani wote awali walijipanga kuihudumia mikoa yote ya Tanzania hadi 2027 kwa kushirikiana na Serikali na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan aliagiza ifikapo Oktoba 2024 wahakikishe wamefika kote na kukabidhi majukumu kwa watendaji wa Serikali ili kujenga tabia ya kujitegemea.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.