• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima ahimiza kilimo Bora cha Pamba Wilaya za Magu na Kwimba

Posted on: August 5th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amewataka viongozi na watendaji wa Halmashauri za Wilaya ya Magu na Kwimba kutoa Elimu ya Kanuni bora za kilimo cha pamba kwa wananchi ili kuwa na ushirikishwaji wa wakulima katika maendeleo ya uzalishaji wa zao hilo.

Ameyasema hayo katika nyakati tofauti  Agosti 05, 2022 alipofika kwenye wilaya hizo kujitambulisha na kutoa dira ya maendeleo katika kuwahudumia wananchi kufuatia kuteuliwa kwake hivi karibuni na Mhe. Rais kuongoza Mkoa huo.

"Napenda kuwapongeza sana Mkurugenzi na timu yako kwa ukusanyaji wa mapato ya ndani hadi mmevuka malengo yenu lakini pamoja na hilo nawaomba tutilie Mkazo zao la pamba ambalo ndio uchumi wa wananchi na sina wasiwasi maana nimeambiwa kuwa shamba darasa la Mkoa lipo hapa" Mhe. Malima akiwa Magu.

Aidha, ametoa rai kwa RUWASA na MWAUWASA kuhakikisha wanaguswa na changamoto ya Maji kwa kila eneo ambalo wananchi wanakosa huduma hizo na amewataka kuweka nguvu kuhakikisha wanaitunza miradi ya maji ili iweze kuwahudumia wañanchi kwa muda mrefu.

Katibu Tawala wa Mkoa, Balandya Elikana amewataka watumishi kwenye Wilaya hizo kufanya kazi kwa bidii ili kuwapa wananchi huduma stahiki ili kutimiza dhima na kiu ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kutaka kuona wananchi wake wanaendelea kiuchumi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Magu Mhe. Salum Kali amemhakikishia kiongozi huyo ushirikiano wa dhati na amebainisha kuwa viongozi ndani ya wilaya hiyo wana ushirikiano wa dhati ambao umezaa Matunda ya kuongoza kwa Ukusanyaji wa Mapato ya ndani kwa Mkoa wa Mwanza.

"Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ametuletea fedha nyingi sana za kutekeleza miradi mingi kwenye kila sekta na tunayo miradi ya kimkakati, tunajengewa hadi shule kubwa ya kisasa kwa Tshs. Bilioni 4 na itakua na uwezo wa kuchukua zaidi ya wanafunzi elfu moja na ukienda kwenye Afya miradi inaendelea." Mhe. Kali.

"Halmashauri ya wilaya ya Kwimba ilikasimia kukusanya Tshs Bilioni 2.4 kwa mwaka wa fedha uliopita na hadi kufikia Juni 30, 2022 tumefanikiwa kukusanya Tshs Bilioni 2.9 sawa na 106% na kwa 2022/23 Halmashauri inakusudia kukusanya Tshs Bilioni 3.1 na tunayo mikakati mbalimbali ya kufikia lengo tulilojiwekea na hata kuvuka lengo." Mkuu wa Wilaya Kwimba.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.