• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AAGIZA KUKOMESHWA KWA UVUVI HARAMU ZIWA VIKTORIA

Posted on: June 6th, 2023

RC MAKALLA AAGIZA KUKOMESHWA KWA UVUVI HARAMU ZIWA VIKTORIA


*Ataka kukomeshwa kwa uvu


*Ataka viongozi kudhibiti Uhamiaji haramu hususani kwenye visiwa*


*Aagiza kurudishwa kwa Mkandarasi aliyejenga barabara Nansio ambayo imebainika kuwa na kasoro*


*Amesisitiza nidhamu kazini pamoja na kushirikiana*


*Awataka Ukerewe kutunza miradi ya kimkakati*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, CPA Amos Makalla leo Juni 06, 2023 amefika Kisiwani Ukerewe akiwa katika Muendelezo wa ziara yake ya kikazi ya kujitambulisha akihakikisha anafika na kuzungumza na Viongozi na Watendaji katika Halmashauri zote za Mkoa huo.


Akizungumza wilayani Ukerewe, Mhe. Makalla ametoa wito kwa wanachi wa Ukerewe kuhakikisha wanafanya shughuli za uvuvi kwa mujibu wa sheria na sio kwa kuharibu mazalia ya samaki aidha ametoa wito kwa Kamati ya Usalama kusimamia hilo wakati wote ili kuimarisha uchumi wa jamii kupitia shughuli za uvuvi.

"Nafahamu ya kwamba Uvuvi ndio shughuli yetu kuu hapa lakini nimekuja kuwakumbusha kuvua kwa kuzingatia sheri tusitumie mabomu, nyavu haramu na aina yoyote ya Uvuvi haramu ili samaki waendelee kuzaliana kwani huo ndio uchumi wetu hivyo tukiharibu tutaharib uchumi wetu." Mhe. Makalla.

Aidha, ameiagiza idara ya Uhamiaji kushirikiana na wananchi hususani kwenye visiwa kuhakikisha hakuna Wahamiaji haramu kwani wilaya hiyo imetawanyika sana kijiografia kwa kuzingatia imezungukwa na visiwa 38 vidogo vidogo vikiwemo 15 vyenye makazi ya kudumu.

Vilevile, amemuagiza Mkuu wa Wilaya kwa kushirikiana na Meneja wa TARURA kuhakikisha mkandarasi aliyejenga barabara ya Mjini yenye urefu wa zaidi ya KM 1 kuhakikisha anaifanyia marekebisho kwenye kasoro zilizobainika ili wananchi wapate mradi wenye kiwango kinachokubalika na thamani ya fedha.

"Mhe. Mkuu wa Wilaya shirikiana na wenzako mrudisheni Mkandarasi aliyejenga barabara ya kiwango cha lami hapa mjini ambayo ina kasoro nyingi na kusababisha manung'uniko kwa wanamchi ili aje aifanyie marekebisho kuondoa kasoro hizo," amesisitiza.

Aidha, Mhe. Makalla amesisitiza kufuatwa kwa taratibu za fedha kwa kukusanya na kuwasilishwa benki kabla ya kuzitumia na akawataka watumishi kushirikiana na Mkaguzi wa ndani wa Halmashauri kujibu hoja za Ukaguzi kwa wakati ili kuifanya Halmashauri hiyo kuenenda kisheria.

Aidha, amesisitiza uadilifu kwa watumishi wa umma katika kuwahudumia wananchi na akatoa wito kwa viongozi kushirikiana na watendahi katika kusimamia miradi ya Maendeleo ili kujenga imani kwa wananchi dhidi ya Serikali yao inayoongozw na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Hassan Bomboko, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe amesema Wilaya hiyo iliyozungukwa na visiwa 38 vidogo vidogo ambapo 15 vina makaazi ya kudumu watu wake wana amani na wanaendelea na shughuli za kujitafutia ridhiki hususani kwa shughuli za uvuvi kwa amani.

Amesema Serikali kuu imekua ikiwajali sana kwani wamepokea zaidi ya Bilioni 12 ndani ya mwaka huu wa fedha kwa ajili ya kutekeleza Miradi mbalimbali katika Sekta za Nishati, Afya, Elimu, Miundombinu na Maji na kwenye hilo amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa niaba ya wananchi wa kisiwa hicho.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.