• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AANDAA MKAKATI KAMAMBE WA KUTATUA KERO ZA WANANCHI

Posted on: September 11th, 2023

RC MAKALLA AANDAA MKAKATI KAMAMBE WA KUTATUA KERO ZA WANANCHI


*Asema siku ya Septemba 18 kuwa Siku ya Uzinduzi wa kusikliza kero za wananchi*


*Aipongeza Serikali ya Rais Samia kuleta miradi mingi ya maendeleo Mwanza*


*Aunda kikosi kazi maalum cha kupokea taarifa za migogoro ya ardhi*


*Awataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuitangaza miradi ya maendeleo kwa wananchi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA. Amos Makalla ametangaza mkakati kamambe wa kutatua kero za wananchi Mkoani humo kwa kuwashirikisha Wakuu wa Wilaya,Wakurugenzi wa Halmashauri na Makatibu Tawala wa Wilaya.

Akizungumza leo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa katika kikao kazi na viongozi hao, Mhe. Makalla amesema atafanya uzinduzi huo Septemba 18 mwaka huu na kuwaagiza Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri,Makatibu Tawala wa Wilaya wahudhurie ili wapate mwongozo mzuri watakapokwenda kushughulika na kero za wananchi.


Mkuu huyo wa Mkoa amesema utaratibu huo ameufanya kwenye mikoa yote aliyofanya kazi hivyo anaamini utaratibu huo kwa Mkoani Mwanza utakuwa na tija kwa Serikali kuwa karibu zaidi na wananchi.

"Nawaagiza viongozi wenzangu mara baada ya uzinduzi huo wa kusikiliza kero za wananchi,muende sehemu zenu za kazi na kuweka mpango kazi wa kuwatembelea wananchi kila kata na baadaye ziwasilishwe kwenye Halmashauri kwa kufanyiwa kazi",amesisitiza CPA Makalla.

Amesema manufaa ya kusikiliza kero hizo zinawapunguzia mzigo wananchi yakiwemo mashauri yaliyopo mahakamani yanayohusu migogoro ya ardhi na mengineyo na kusisitiza utaribu huo usiishie kusikiliza tu bali pia kutoa majibu, kushauri na mwelekeo wa jambo husika.

Amewaagiza pia watumishi wa Idara za ardhi kwenye Halmashauri waweke utaratibu wa kuwahudumia wananchi hasa migogoro ya ardhi na mipaka.


"Nimeunda kikosi kazi maalum ambacho kitapita kwenye Halmashauri zote kupata taarifa za migogoro ya ardhi niwaombe viongozi wote mtoe ushirikiano kwa kiosi kazi hiki",CPA Makalla

Ameongeza kuwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi waunde timu ya pamoja na kuitangaza bayana miradi yote ya maendeleo kwa wananchi na kusikiliza changamoto na muendelezo wa miradi hiyo na shule zote na hospitali ziwe na mipaka ili kuepuka kuingiliwa.

Mkuu huyo wa Mkoa amesisitiza Mkoa wa Mwanza bila kero za wananchi inawezekana na kazi hiyo ikifanyika kikamilifu itaondoa malalamiko kwa viongozi wa Kitaifa wanapofanya ziara.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.