• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AFURAHISHWA NA MWENENDO MZURI WA PAMBA JIJI FC, AWAMWAGIA MINOTI

Posted on: January 26th, 2024

RC MAKALLA AFURAHISHWA NA MWENENDO MZURI WA PAMBA JIJI FC, AWAMWAGIA MINOTI


*Awajaza Shs Milioni 5 kama motisha ya kuiangamiza Biashara FC*


*Atangaza tarehe 3 Februari 2024 kuwepo Harambee ya kuichangia Pamba Jiji FC*


*Awahimiza kukaza buti uwanjani kutimiza malengo ya kucheza Ligi kuu msimu ujao*


Leo Januari 26, 2024 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla amefanya mkutano wa kawaida na wachezaji na timu ya soka ya Pamba Jiji FC na kuwakabidhi kibunda cha Milioni 5 kama motisha ya kuendelea kutoa dozi dimbani katika michezo yake ya Ligi ya Championship.


Mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi yake ulioambatana na chai ya pamoja, Makalalla ambaye pia ni mlezi wa timu hiyo amebainisha amezidi kukunwa na kiwango cha timu hiyo na muendelezo wa ushindi katika michezo yao.

"Mimi ugonjwa wangu ni mpira wa miguu mkinifurahisha katika eneo hili nanyi mtaona matunda yake,hongereni sana kwa kiwango kizuri mlichoonesha katika mpambano wenu dhidi ya Stendi Utd". Mkuu wa mkoa

Amesema mchezo ujao dhidi ya Biashara United kutoka Mara hana shaka ya kushuhudia pointi nyingine 3 zikiendelea kuvunwa na kuzidi kujiimarisha nafasi ya juu katika msimo wa Ligi hiyo.

"Niliwaleta wachezaji 5 kutoka Congo DRC kwa majaribio lakini mwisho wa siku wote hawakuonesha kiwango cha kulishawishi dawati la ufundi kuwasajili,lakini nyie baadhi yenu tuliowaongeza dirisha dogo mpo vizuri hongereni",amesisitiza mlezi huyo aliyecheza pia soka miaka ya nyuma.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema ili kuhakikisha wana TP Lindanda wanazidi kuwa tishio mwanzoni mwa mwezi ujao ataandaa harambee ya kuichangia timu hiyo lengo ni kuzidi kuwapa hamasa na motisha wachezaji hao ili kutimiza malengo ya kucheza Ligi kuu msimu ujao.

Amezidi kuwakumbusha wananchi wa Mwanza kuendelea kushikamana na kuwapa ari wachezaji wa Pamba Jiji FC kwa kujitokeza kwa wingi dimbani katika michezo yake ya nyumbani na hata ugenini


"Hiki unachokifanya Mhe.Mkuu wa Mkoa hata mimi unanirahisishia kazi yangu yaani inakuwa nyepesi kutokana na wachezaji ari ya kujituma na kuyashika maelekezo ya kiufundi inakuwa nzuri,"Mbwana Makatta,kocha wa Pamba Jiji FC


Katika msimamo wa Ligi ya Championship wana TP Lindanda wanashikilia nafasi ya pili na mtaji wa pointi 40 kibindoni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.