• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AIKABIDHI RASMI HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA TIMU YA SOKA YA PAMBA FC

Posted on: July 14th, 2023

*RC MAKALLA AIKABIDHI RASMI HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA TIMU YA SOKA YA PAMBA FC*


 *Asema kipaumbele chake ni Mwanza kuwa na timu ya Ligi Kuu**


 **Mwanza ina vipaji vya soka,viwanja vizuri vya mpira na Chuo cha michezo Malya.*


*Uendeshaji Michezo inahitaji fedha pia michezo inachochea uchumi na Utalii wa michezo.*


 *Awaomba wananchi Mkoa wa Mwanza kuwa Na Umoja*


Halmashauri ya Jiji la Mwanza leo Julai 14,2023 inatarajia kupokea barua rasmi ya kukabidhiwa na kuiendesha  timu ya soka ya Pamba FC maarufu kama TP LINDANDA kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza baada ya mchakato wa umiliki kutoka bodi ya Pamba na kuletwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kukamilika.

Akizungumza leo na wadau wa michezo kwenye ukumbi mkubwa wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla amebainisha Mkoa huo una kila sababu ya kuwa na timu ya Ligi kuu kutokana na historia yake nzuri ya kuwa na vipaji vya soka na miundombinu bora ya viwanja.

Amesema baada ya kukabidhiwa rasmi timu ya Pamba kwa barua alikutana na uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza chini ya Mkurugenzi Aaron Kalugumjuli na kuwauzia wazo la kuimiliki na kuiendesha na walikubali kwa mikono miwili,hivyo leo baada ya kikao hicho atamkabidhi naye rasmi kwa barua.

"Ndugu zangu nimewaita hapa wengi wenu mnajua mimi ni mdau kindaki ndaki wa soka nikianzia kuucheza kwa muda mrefu katika mpira wa kisasa huwezi kufanikiwa kwa vimichango vidogo vidogo ni lazima sasa tuingie katika sura mpya sitakuwa nautendea haki Mkoa huu kama tutakosa timu ya Ligi Kuu",amesisitiza CPA Makalla.

Katika Mkutano huo uliohudhuriwa na viongozi wa Chama cha Soka Mwanza na uongozi wa timu ya Pamba,Mkuu huyo wa Mkoa amehimiza mchakato wa kuundwa kamati ya mpito kwa lengo la kukamilisha hatua zote muhimu za usajili na mapendekezo ya kocha wachezaji gani wabaki na nani wakuwachwa yafanyike haraka.

" Tuutumie muda huu mchache vizuri kuanzia marekebisho ya benchi la ufundi,na tuangaze baadhi ya wachezaji bora wa Ligi kuu waje kuchanganyika na hawa ili tupate timu imara itakayo kuja kuutoa kimaso maso Mkoa wa Mwanza," amehimiza Mkuu huyo wa Mkoa.

"Sisi kama viongozi wa soka Mkoani hapa,hatua hii imetufariji na mwanga wa kucheza Ligi kuu tunauona, hasa ikizingatiwa kuendesha timu kwa mafanikio kuna hitaji fedha nyingi," Vedasto Lufano,M/kiti MZFA.

"Hadi leo tulikuwa tumejichangisha Shs Milioni 14 kwa ajili ya kuiendesha timu msimu huu,lakini kwa taarifa hii timu ya kuwa chini ya Halmashauri ni dhahiri tutafika mbali,tunakushukuru mno Mhe. Makalla,"Evaristi Hagilla,M/kiti Klabu ya Pamba

Kwa zaidi ya miaka 20 timu ya soka ya Pamba haijashiriki Ligi Kuu licha ya kutamba miaka ya 90 na kutoa wachezaji wengi waliong'ara kwenye vilabu vikubwa vya Simba na Yanga akiwemo George Masatu.Hussein Marsha,John Makelele na Fumo Felician.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.