• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AMEWATAKA WANANCHI KULINDA VIFAA VYA MRADI WA SGR

Posted on: June 2nd, 2023

RC MAKALLA AMEWATAKA WANANCHI KULINDA VIFAA VYA MRADI WA SGR


*Aomba ushirikiano katika kuwaletea maendeleo wananchi*


*Aipongeza Kwimba kwa mafanikio, aiangazia michezo*


*Asisitiza kudumishwa kwa Usalama kwa wananchi*


*Awataka viongozi kutoa elimu dhidi ya madhara ya imani za Kishirikina*


*Ana imani kubwa na nidhamu kazini kama dira ya Maendeleo*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutekeleza miradi ya kimkakati nchini hususani mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) na amewataka wananchi kulinda Miundombinu hiyo kizalendo ili ufikie adhama ya kukuza uchumi wa nchi.

Akizungumza na viongozi, watendaji na makundi mbalimbali leo tarehe 02 Juni, 2023 kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba Mhe. Makala amesema uchumi wa nchi utakua zaidi kupitia Miradi ya kimkakati hivyo ni lazima wananchi wawe wazalendo kuilinda kusiwe na upotevu wa vifaa wakati wa utekelezaji.

"Tukiruhusu wizi wa vifaa na mafuta kwenye miradi yetu tunajiibia wenyewe na tunajichelewesha kupata maendeleo, nawaomba wana Kwimba tulinde mradi wa SGR na tuhakikishe vifaa kwenye kambi ya Ujenzi iliyopo hapa haviibiwi kwani mradi huo ukikamilika tutasafirisha Pamba kwa haraka sana na tutakuwa kiuchumi." CPA Makalla.

Aidha, ametumia wasaa huo kuomba ushirikiano kwa viongozi na watumishi wote huku wakitanguliza nidhamu mahala pa kazi ili kwa pamoja waweze kumsaidia Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kuwaletea maendeleo wananchi katika kila sekta hususani za kilimo, uvuvi, uchimbaji madini na biashara.


Vilevile, ameipongeza wilaya hiyo kwa mafanikio na maendeleo makubwa waliyofikia tofauti na siku za nyuma na kwamba amewataka kuendelea kudumisha amani ili kuhakikisha wananchi wanakuwa na uhuru wa kufanya kazi za maendeleo na kuacha tabia za kufanya ramli chonganishi.

"Inashangaza kuona Chuo cha michezo nchini kipo hapa Kwimba kinaitwa Malya ila Mkoa huu hauna timu kwenye ligi kuu, ni lazima tufanye mageuzi kwenye michezo ili chuo hiki kitunufaishe kwanza sisi wenyewe na turudishe furaha kwa wananchi wa Mwanza", Mhe. Makalla akizungumzia Michezo.


Naye, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija amesema wananchi wa wilaya hiyo wanaendelea na uzalishaji ambapo kwa sasa wapo kwenye mavuno ya Pamba, Mahindi na Mpunga lakini vilevile wanalima choroko kwa amani kutokana na kazi nzuri inayofanya na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Sungusungu.

"Tunaendelea kufanya mikutano kwa wananchi tukiwakumbusha kutunza chakula kwa ajili ya siku za baadae kwani kwa kuzingatia historia ya msimu uliopita hawakufanikisha mavuno mengi hivyo ni lazima kuweka akiba na tunahakikisha pembejeo za kilimo zinawafikia wakulima wetu kwa wakati," amesema Mhe. Ludigija

Ameongeza kuwa kwa mwaka wa fedha uliopita Halmashauri hiyo ilitengewa Bilioni 20 kutekeleza miradi ya maendeleo na  hadi sasa wamepokea zaidi ya fedha hizo lakini vilevile Halmashauri hiyo inayotegemea kukusanya kupitia kilimo wameshakusanya Bilioni 3.2 ambapo ni sawa na 97% ya makadirio.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS MWANZA ATAKA UHAMASISHAJI CHAKULA CHENYE LISHE KUONGEZEKA SHULENI

    May 13, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BONDE LA ZIWA VICTORIA KWA KUELIMISHA UMMA

    May 13, 2025
  • RC MTANDA ASISITIZA UIMARISHWAJI WA UMOJA NA MSHIKAMANO

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.