• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA APIGA KAMBI YA SIKU TATU VISIWA VYA UKEREWE

Posted on: November 21st, 2023

RC MAKALLA APIGA KAMBI YA SIKU TATU VISIWA VYA UKEREWE


*Amshukuru Rais Samia kwa kutoa Bilioni 34 Kujenga Vivuko Vipya kuboresha Usafiri visiwani*


*Amshukuru pia kwa Kujenga Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwenye Wilaya hiyo iliyo kisiwani*


*Makalla afafanua kuwa zaidi ya Bilioni 22 zitatumika kuboresha huduma za Maji kisiwani Ukerewe chini ya RUWASA*


*Abainisha kuwa Rais Samia atoa Bilioni 130 kupeleka Umeme Ukerewe*


*Awaagiza Halmashauri ya Ukerewe kutoa kipaumbele kwa wazabuni wazawa*


Leo jumanne Novemba 21, 2023 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amefika Kisiwani Ukerewe kwa ziara ya Siku tatu ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na ukaguzi wa Miradi ya maendeleo ambapo anatarajia kufika kwenye baadhi ya Visiwa kikiwemo  Ukara.

Akizungumza na wananchi wa wilaya hiyo, Mhe. Makalla amempongeza Rais Samia kwa kuboresha huduma za usafiri wa Majini kwa kutoa Bilioni 34 kujenga vivuko vipya 10 mkoani huko kikiwemo cha Rugezi- Kisorya wilayani Ukerewe ambacho ifikapo mwezi Aprili 2024 kitaanza kutumika na kusaidia kuimarisha usalama wa abiria.


Amesema kuwa Rais Samia amekua mlezi bora kwa kujali wananchi wake kwani anahakikisha anaboresha maisha ya kila mtanzania kwa kupeleka huduma bora kila kona na ndio maana wananchi hususani wa visiwani kama Ukerewe na Visiwa vingine 38 vinavyozunguka wilaya hiyo ameamua kuwapelekea vivuko vipya ili wawe salama wakati wote wanaposafiri.

Vilevile, Mhe. Makalla amesema wananchi zaidi ya 887,000 wa Wilaya hiyo siku za karibuni watanufaika na huduma za Kibingwa za afya kutokana na kujengewa hospitali ya Rufaa yenye hadhi ya Mkoa na kwamba tayari zaidi ya shilingi Bilioni nne zimepelekwa na ujenzi umeanza.


Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amendelea kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kudhamiria kumaliza tatizo la nishati ya Umeme na ameshatoa Bilioni 130 kwa ajili ya Ujenzi wa mradi mkubwa na kwamba mkandarasi ameshapatikana ambaye atajenga miundombinu kwa kilomita 98 pamoja na kituo cha kupoza umeme.

"Rais Samia anawapenda wananchi wa Ukerewe, jiandaeni na umeme wa uhakika na mkandarasi ameshapatikana na siku za karibuni ataanza kazi na kambi yake itakua kwenye kijiji cha Malegea", amefafanua Mhe. Makalla wakati akielezea mradi utakaohusisha njia ya usafirishaji yenye umbali wa Kilomita 98 pamoja na kituo cha Kupoza umeme.

Halikadhalika, CPA Makalla amebainisha kuwa wananchi wa Nansio, Ukara, Bukindo, Irugwa, Sizu na Gana wanajengewa miradi mikubwa ya maji ambayo ukamilifu wake utawapatia maji aafi na salama na kuimarisha afya na kwamba itaondoa adha hiyo kwa wananchi.

Akijibu kero zilizowasilishwa na Ndugu Leberatus Mulebele Mhe. Makalla amewataka Halmashauri ya Ukerewe kutoa zabuni kwa wafanyabiashara wazawa ili kuwainua kiuchumi na kuhakikisha wanatoa muongozo wa uchangiaji kwa wananchi kwenye huduma za usafiri wa gari la wagonjwa na inapotokea rufaa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.