• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AZIDI KUWAJAZIA MAPESA PAMBA JIJI FC SASA KILA GOLI ANUNUA KWA MILIONI MOJA

Posted on: March 27th, 2024

RC MAKALLA AZIDI KUWAJAZIA MAPESA  PAMBA JIJI FC SASA KILA GOLI ANUNUA KWA MILIONI MOJA


*Awapongeza matokeo ya mchezo wa ugenini dhidi ya Kengold*


*Awataka kukaza buti michezo minne iliyosalia*


*Awasihi kuepuka kurubuniwa na kusaliti timu*


Wakati filimbi ya kuhitimishwa michuano ya ligi ya Championship ikiwa ukingoni kupulizwa, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amezidi kuwapa ari wachezaji wa timu ya Pamba Jiji FC kwa kununua kila GOLI Sh. Milioni moja kwa michezo yao minne iliyosalia.

Makalla ambaye ni mlezi wa timu hiyo amesema hayo leo Machi 27, 2024 alipowatembelea wachezaji wa Pamba Jiji kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana, amesema mbali ya motisha hiyo pia amewapa Sh. Milioni 5.2 kama bonus yao kutokana na mwenendo mzuri na kucheza soka la kiwango hasa katika mpambano wa ugenini dhidi ya Kengold.

"Mimi sina maneno mengi zaidi ya kuwa mtu wa vitendo kama nilivyowaahidi,ule mchezo dhidi ya Kengold mliwafanya wenyeji wenu kama wapo ugenini kutokana na soka mliowatandazia na mwishowe tukatoka share ya 2-2 na kupata alama moja ambayo imetuweka pazuri", CPA Makalla.

Makalla ambaye ni mkereketwa wa soka ametaka Pamba Jiji FC kuwa na juhudi zaidi uwanjani kwa kufunga mabao mengi na hatakuwa na hiana kwenye kutoa fungu la pesa la magoli hayo  na kuwasisitiza kutokubali kuruhusu mabao ya kufungwa.

"Hapa naomba tuelewane mkishinda 3-2 hapo natoa milioni moja tu kutokana na kuruhusu magoli mengi ya kufungwa,safu ya ulinzi na mabeki nataka kuona ukatili wa kutoruhusu mpinzani kuwapenya na kuwafunga," amehimiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Katika mazungumzo hayo na wachezaji Makalla amewataka kutanguliza uzalendo na kutokubali kurubuniwa hasa kwa kipindi hiki cha michuano kuelekea ukingoni kutokana na timu zilizowakaribia kuweza kufanya fitna ili zipate nafasi.

Nahodha wa timu hiyo na mchezaji mkongwe Jerryson Tegete amemuhakikishia mlezi wao sasa wachezaji wote wsmeshaona njia nyeupe ya kucheza ligi kuu nsimu ujao,hivyo wataendelea kuzingatia maelekezo yote kuanzia kwake na dawati lao la ufundi.

Timu ya soka ya Pamba Jiji FC hadi sasa imejikusanyia kibindoni point 55 baada ya kucheza michezo 26 na kushika nafasi ya pili nyuma wa vinara wa kundi hilo Kengold wenye pointing 60 na Jumamosi watawaalika Polisi Tanzania mpambano utakaorindima kwenye uwanja wa Nyamagana.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.