• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima ahimiza Sensa ya Watu na Makazi Mwanza

Posted on: August 4th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amewataka viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuweka mkazo kwenye zoezi la Sensa ya watu na Makazi linayotarajia kufanyika jumanne ya Agosti 23, 2022 nchini ili lifanikiwe kwa kiwango kilichokusudiwa.

Mhe. Malima amesema hayo  Agosti 03, 2022 wakati akizungumza na Viongozi, watumishi na wadau wa maendeleo wilayani  Nyamagana akiwa kwenye ziara ya kujitambulisha na kupata taarifa ya Maendeleo kufuatia kuteuliwa kwake kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza mwishoni mwa wiki.

Aidha, Mhe Malima amesema amefurahishwa na mwenendo wa Ukusanyaji wa mapato ya ndani kwenye Halmashauri hiyo na ametoa wito kwa Watumishi kuhakikisha wanaongeza wigo wa Ukusanyaji wa mapato na kuboresha upatikanaji wa huduma bora kwa jamii kama vofaa tiba kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya.

"Wananchi wa Nyamagana wamewakabidhi hatma ya maisha yao, nendeni mkaonekane kwenye Ukusanyaji wa Mapato, utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kupunguza hoja za mdhibiti na mkaguzi wa Hesabu za Serikali maana mimi nachukia sana kuwepo kwa hoja za kizembe kutokana na kutokujali." Mhe. Malima.

Aidha, ameagiza kupatiwa taarifa ya utekelezaji wa zoezi la mikopo ya asilimia kumi kwa makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kutoka sehemu ya Ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri kwani ni kiu yake kuona usimamizi wa dhati kwenye eneo hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amesema Ukusanyaji wa Mapato 2021/22 Halmashauri ya Jiji la Mwanza wamekusanya Zaidi ya Bilioni 18 sawa na Asilimia 103 ya makisio na wamekua wakitekeleza Miradi kadhaa ya kimkakati ukiwemo Mradi wa Stendi ya kisasa ya Nyegezi inayotekelezwa kwa Bilioni 23 ikiwa imefikia 76 ya utekelezaji.

Aidha, amesema Wilaya hiyo kupitia Halmashauri ya Jiji imekua ikitekeleza kwa dhati miradi mbalimbali ya Maendeleo katika sekta za Elimu, Afya, Uvuvi, Ufugaji na Miundombinu ambako kote wamekua mstari wa mbele kuimarisha jamii kwa kuwajengea uwezo katika shughuli wanazofanya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.