• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima aitaka Sekta ya Maji kuboresha huduma Mwanza

Posted on: October 25th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amezitaka taasisi zinazosimamia maendeleo ya Sekta ya Maji mkoani humo kuboresha huduma hiyo kwa wananchi ili kuondoa kero ya upatikanaji wa maji pungufu kwenye jamii.

Mhe. Malima amebainisha hayo leo Oktoba 25, 2022 wakati wa kikao kilichowakutanisha Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA), Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira vijijini (RUWASA) na Mamlaka ya Huduma za Maji mjini Sengerema (SEUWASA) kufanya tathmini ya Maendeleo ya Miradi ya Maji Mkoani humo.

Mhe. Malima amesema kufuatia kuibuka kwa malalamiko kutoka kwa wananchi dhidi ya huduma duni ya Upatikajai wa Maji wakati wa ziara ya Mhe. Abdulrahman Kinana (Makamu Mwenyekiti CCM Bara) Mkoani humo,  imemsukuma kuziangalia kwa karibu taasisi zinazoshughulika na Maji ili kuhakikisha uzalishaji wa unaboreshwa mara moja.

Vilevile, ameagiza umakini na ufanisi katika utekelezaji wa miradi ili kuondoa upotevu wa Maji uliofikia hadi asilimia 32 kwenye Mradi Mkubwa wa chanzo cha Kapripoint wenye uwezo wa kuzalisha lita Milioni 90 kwa siku lakini wanazalisha pungufu na kusababisha maeneo mengi ya wakazi wa Mji wa Mwanza kukosa maji ya kutosha.

Mhandisi Leonard Msenyele, Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA akiambatana na wakandarasi na wafadhili wa mradi mkubwa wa Maji wa Butimba unaotarajia kuzalisha Lita Milioni 48 kwa siku amesema ujenzi wa mradi huo unaendelea vizuri na kwamba wananchi watapata huduma iliyoboreshwa kwa wakati kadiri ya mkataba na kwamba mradi huo utaongeza huduma hiyo kwa wananchi.

Kaimu Mkurugenzi wa MWAUWASA Mhandisi Salim Lossindilo amefafanua kuwa kuna tatizo la uchakavu wa mitambo linalokadiriwa kuhitaji Tshs Bilioni tatu ili kuondoa tatizo hilo na kwamba wanaendelea na jitihada za kupata pampu zitakazosaidia kuongeza nguvu kwenye vituo vya usambazaji vya Mabatini, Kona ya Bwiru na Nyegezi ili wananchi wanaoishi pembezoni wapate maji ya kutosha.

"Tatizo la Mji wa Mwanza Mkuu wa Mkoa ni kwamba upo kama bakuli kijografia, yaani usambazaji wa maji unakua mgumu sana kwa wananchi wanaoishi pembezoni na kwenye maeneo ya miinuko na hali hii tutaiondoa kwa kuboresha Miundombinu yetu kuwa imara zaidi wakati wote tofauti na hivyo wakazi wanaoishi kwenye maeneo tambarare na chini watanufaika zaidi." Amefafanua Mhandisi Lussindilo.

Amefafanua kuwa lengo la ukarabati huo ni kuhakikisha wanajaza matanki ya pembezoni kama Nyashana ambalo sasahivi linaingizwa maji kwa asilimia 50 tu na kwamba baada ya kupata mitambo hiyo huduma ya maji kwa wananchi wanaoishi kwenye maeneo yenye miinuko itaimarika kwani uzalishaji na usambazaji utaongezeka.

Meneja wa Ruwasa Mkoa Mhandisi Exaud Humbo amesema pamoja na kutekeleza miradi ya zaidi ya Bilioni 112 kwa mwakq 2022/23 wana changamoto ya Msamaha wa Kodi hali inayopelekea Miradi kuchelewa kuanza taratibu za manunuzi ambapo kati ya Miradi 29 ni sita tu imepata msamaha na kwamba kumekua na tatizo la wakandarasi kuzembea kazi.

Naye, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Ambrose Pascal amefafanua kuwa Wizara ya Ujenzi na Mfuko wa Barabara wameshatoa zaidi ya Bilioni 10 kwa ajili ya Ujenzi wa Daraja la Simiyu lililopo Magu ili kuimarisha mawasiliano kwenye eneo hilo ambalo wakazi wake wanatumia daraja jembamba lililojengwa miaka mingi iliyopita na kwamba taratibu za utekelezaji zimeanza.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.