• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AAGIZA UCHUNGUZI KUBAINI CHANZO CHA MOTO KITUO CHA AFYA KAKOBE

Posted on: September 2nd, 2024

RC MTANDA AAGIZA UCHUNGUZI KUBAINI CHANZO CHA MOTO KITUO CHA AFYA KAKOBE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa muda wa siku kumi na nne kwa Katibu Tawala Mkoa huo Bwana Elikana Balandya kuunda timu maalumu ya kuchunguza chanzo cha tukio la moto lililotokea usiku wa kuamkia September 02 katika kituo cha afya Kakobe kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo leo Septemba 02, mara baada ya kutembelea kituo hicho  na kujionea madhara yaliyotokana na moto huo, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wananchi hao kuwa na subira katika kipindi hiki ambapo Serikali inaendelea kutafuta namna mbadala ya kuwapatia wananchi hao huduma muhimu ya matibabu.

Akiwatoa hofu wananchi zaidi ya elfu 20 wanaotumia kituo hicho, RC Mtanda amesema huduma zitaendelea kutolewa kama kawaida kwani Mganga Mkuu wa Mkoa atahakikisha anachukua hatua za dharula ili kuhamishia huduma za maabara kwenye jengo linalofaa.

Aidha, amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa kufanya tathmini kwenye uharibifu wa majengo hayo na kushauri kama yanastahili kukarabatiwa au vinginevyo ili hatua zichukuliwe mara moja za kuhakikisha huduma zinarejeshwa kwenye kata hiyo ya Kazunzu.

Akitoa taarifa ya tukio hilo la moto, Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt. Vita Ndohele amesema chanzo cha moto huo inasemekana ni hitilafu ya umeme katika chumba cha maabara na kupelekea kuungua kwa jengo la wagonjwa wa nje ambalo lina vyumba saba, kuteketea kwa vifaa tiba pamoja na dawa vilivyokua vikitumika ndani ya vyumba hivyo huku hasara ya dawa na vifaa tiba ikisemekana kuwa ni zaidi ya thamani ya shilingi Milioni 100.

Halikadhalika, amewashukuru wananchi kwa utulivu na ushirikiano katika kuokoa vitu visiteketee mara tu baada ya madhira hayo kutokea majira ya saa 7 usiku wa kuamkia leo kabla ya Taasisi ya uokoaji ya zimamoto kuwasili kwa msaada zaidi kutokana na umbali uliopo kutoka Mkoani.

Kituo hicho kilichoanzishwa tangu mwaka 1986 kimekua tegemeo kwa zaidi ya wananchi elfu 20 kutoka kwenye tarafa nzima ya Kakobe.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.