• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AHIMIZA WELEDI KWA WAKANDARASI WAZAWA MIRADI YA SERIKALI,AZITAKA TAASISI KUJENGA VIWANJA VYA MICHEZO

Posted on: August 5th, 2024

RC MTANDA AHIMIZA WELEDI KWA WAKANDARASI WAZAWA MIRADI YA SERIKALI,AZITAKA TAASISI KUJENGA VIWANJA VYA MICHEZO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda leo Agosti 5,2024 amefanya ziara fupi ya ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa Taasisi ya Teknolojia Dar-e-s Salaam Tawi la Mwanza unao gharimu shs bilioni 37 unatekelezwa na Mkandarasi mzawa Kampuni ya Comfix Engineering na kuhimiza weledi katika miradi ya Serikali.

Mkuu huyo wa Mkoa akiwa na mkurugenzi wa tawi hilo Dkt.Albert Mmari amejionea hatua ya umaliziaji wa majengo manne ya ufundishaji,Taaluma na hosteli za wanaume na wanawake pamoja na uwanja wa michezo wa siku nyingi wa tawi hilo na kutaka uboreshwe ili uje kuwa na tija zaidi.

"Nimefurahishwa na uwanja huu na hapa naomba nitoe msisitizo,Taasisi zote za Serikali na binafsi jengeni viwanja vya michezo nchi yetu ipo mbioni kuwa mwenyeji wa michuano ya AFCON 2027 na huenda CCM Kirumba ukatumika mtajiongezea vipato timu zikija kufanya mazoezi,"amesisitiza Mtanda.

Amesema katika michuano ya ligi kuu ya NBC timu mbalimbali zitafika kucheza na Pamba Jiji FC na wakati zinajiandaa na mechi zitahitaji viwanja vya mazoezi.

Akizungumza kampuni za watanzania kupewa miradi mikubwa ya Serikali,Mtanda amesema ni wajibu wao kutanguliza uaminifu na kuikamilisha kwa wakati hali ambayo itawajengea kuaminiwa na Serikali.

"Huu mradi wa miundombinu hii uliogharimu fedha nyingi ni mfano mzuri kwa mkandarasi huyu,kila jengo naambiwa linakamilika mwaka huu,endeleeni na weledi huu,"Mtanda

Kwa upande wake mkurugenzi wa tawi hilo Dkt.Albert Mmari amesema ujenzi huo una malengo makuu matatu kuongeza udahili,kuongeza programu ya elimu ya ufundi na ushirikiano wa kikanda.

"Mara baada ya mradi huu kukamilika utakuwa na tija kwa nchi za Afrika Mashariki na kati kwa watu kuja kupata utaalamu wa juu namna ya kuzalisha bidhaa za ngozi,"Dkt.Mmari

Ujenzi huo wa majengo ya kisasa ulioanza mwaka 2019 na utakamilika mwaka huu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.