• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AIHAKIKISHIA TUME HURU YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MWANZA

Posted on: August 9th, 2024

RC MTANDA AIHAKIKISHIA TUME HURU YA UCHAGUZI USALAMA WA UCHAGUZI MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameiambia Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Mkoa wa Mwanza haujawahi kukwamisha shughuli au jambo lolote ambalo serikali imelipanga,  kwa maanaa hiyo pia hata uchaguzi Mkoani humo utakuwa wa amani na utulivu.

Mhe. Mtanda ameyasema hayo mapema leo Agosti 09, 2024 wakati alipokuwa akiipokea na kuikaribisha Mkoani Mwanza Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi iliyowasili Mkoani hapo kwa ajili ya mkutano wa tume na wadau wa uchaguzi kuhusu uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesema serikali ya Mkoa tayari imeshaanza  kuifanya kazi hiyo kwa kutoa elimu ya uchaguzi na upigaji kura kwa wananchi kupitia mikutano mbalimbali ambayo imekuwa ikifanyika Mkoani humo na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika vituo mbalimbali vitakavyoainishwa ili warekebishe na kuandika taarifa zao.

"Tumejipanga kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani, na kuanzia sasa niseme tu ofisi yangu itatoa ushirikiano wa kutosha mpaka pale uchaguzi utakapokamilika".

Naye Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele amesema wamedhamiria kufanya maandalizi ya kutosha kuelekea uboreshaji wa daftari la kudumu la mpiga kura na kwa Mkoa wa Mwanza wameanza na mkutano huo utakaowashirikisha wadau wa uchaguzi ambao ni vyama vya siasa, dini, asasi na makundi mbalimbali.

"Tume imeendelea na maandalizi mbalimbali ikiwemo ya kutoa elimu ya upigaji kura kupitia vyombo mbalimbali vya habari, mikutano ya hadhara, pamoja na kutumia magari ya matangangazo". Amesema Mhe. Jaji Mwambelege.

Aidha Mwenyekiti wa Tume hiyo pia amemtaka Mkuu wa Mkoa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha elimu inasambaa zaidi kwa wadau wote kwa kuwa ana wasaidizi wengi hususani katika maeneo ya ngazi za chini za utawala.

Uboreshaji wa daftari la mpiga kura kwa Mkoa wa Mwanza unatarajiwa kuanza rasmi kuanzia 21 - 28 mwezi Agosti 2024.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.