• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AINGILIA FEDHA MIL.79 ZA HOSPITALI YA UKEREWE, ATOA SIKU 3 KWA MKAGUZI

Posted on: February 9th, 2026

Bakaa ya shilingi milioni 79 iliyosalia baada ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe imeibua maswali kuhusu uwazi wa matumizi ya fedha za umma, hali iliyomlazimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, kuingilia kati na kuagiza ukaguzi wa haraka wa fedha hizo.

Akizungumza wakati wa ziara yake ya ukaguzi hospitalini hapo, Mhe. Mtanda amesema fedha hizo ni salio la mradi wa ujenzi wa hospitali, lakini hadi sasa hakuna mpango ulio wazi unaoeleza namna zilivyopangwa kutumika, jambo alilolitaja kuwa ni kinyume na misingi ya uwajibikaji na usimamizi wa fedha za Serikali.

Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa Mkoa amemuelekeza Mkaguzi wa Ndani kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kuwasilisha ripoti ya kina inayoeleza chanzo, mpango na matumizi yaliyopangwa ya fedha hizo ndani ya siku tatu.

“Ninajua fedha hizi zipo kama bakaa ya ujenzi wa hospitali, lakini matumizi yake hayajawekwa wazi kwa kiongozi yeyote. Haiwezekani kuendelea kuomba fedha mpya kutoka Serikalini ilhali fedha zilizopo bado hazina matumizi yanayoeleweka. Mkaguzi alete ripoti tujue ukweli,” amesisitiza.

Ameonya kuwa nidhamu na uwazi wa matumizi ya fedha za umma ni jambo lisilojadilika, akisisitiza kuwa viongozi wanapaswa kusimamia fedha kwa uadilifu ili kuleta matokeo chanya kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mtanda ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kwa kutekeleza maelekezo aliyoyatoa awali, ikiwemo kukamilisha jengo la mama na mtoto pamoja na kufanya tathmini ya majengo ya hospitali ambayo hayajakamilika.

Amesema tathmini hiyo ni muhimu katika kuiwezesha halmashauri kuandaa maombi ya fedha za ukamilishaji kutoka Serikali Kuu ili kuhakikisha miundombinu ya hospitali inakamilika na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Sambamba na hayo, Mkuu wa Mkoa amekagua mradi wa mtambo wa kuzalisha oksijeni katika hospitali hiyo na kuishukuru Serikali kwa kufanikisha utekelezaji wa mradi huo, akisema umeleta manufaa makubwa kwa wananchi wa Wilaya ya Ukerewe, hususan katika kuboresha huduma za afya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AINGILIA FEDHA MIL.79 ZA HOSPITALI YA UKEREWE, ATOA SIKU 3 KWA MKAGUZI

    February 09, 2026
  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127

    February 09, 2026
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI

    February 09, 2026
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU

    February 06, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.