• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AIPONGEZA DORIS MOLLEL FOUNDATION KWA MRADI WA BILIONI 2 WA WODI YA WATOTO WACHANGA KWIMBA

Posted on: February 19th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Doris Mollel Foundation kwa kutoa shilingi bilioni 2 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Wodi ya Watoto Wachanga (Neonatal Care Unit) katika Wilaya ya Kwimba. Amesema kiwango cha ubora wa mradi huo ni cha juu na kinaleta matumaini mapya kwa huduma za afya mkoani humo.

Akizungumza Februari 19, 2026 wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi wa mradi huo Kwimba, Mhe. Mtanda amesema sasa watoto wachanga watapata matibabu sahihi na ya kisasa. Ameongeza kuwa pamoja na ubora wa jengo, huduma zitakazotolewa zitakuwa bora na imara, kwani tayari timu ya madaktari bingwa imeanza maandalizi ya utoaji huduma.

Amesema katika mwaka wa fedha 2025/2026, Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba imepokea shilingi milioni 774.4 kwa ajili ya miundombinu ya sekta ya afya. Aidha, upatikanaji wa bidhaa za afya katika halmashauri umefikia asilimia 90, huku upatikanaji wa dawa mkoani Mwanza ukiwa asilimia 93 baada ya Serikali kuleta shilingi bilioni 1.2 kuboresha huduma hizo.

Mhe. Mtanda ametoa wito kwa wananchi kutunza na kuhifadhi miundombinu ya afya iliyojengwa ili iweze kudumu na kuendelea kutoa huduma bora kwa jamii. Amesisitiza kuwa uwekezaji huo una lengo la kupunguza vifo vya watoto wachanga na kuboresha viwango vya maisha.

Akisoma taarifa ya mradi, Msimamizi wa mradi huo, Mhandisi Alistides Leopord Kahigimo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba, amesema ujenzi unatekelezwa na Doris Mollel Foundation kwa ufadhili wa taasisi ya Keep a Child Alive ya nchini Marekani, iliyoanzishwa na msanii Alicia Keys.

Mradi huo unatekelezwa na mkandarasi Kiure Construction Company Limited na ulianza Mei 6, 2025, ukitarajiwa kukamilika ifikapo Februari 22, 2026. Hadi sasa umefikia asilimia 99.5, huku kazi zinazoendelea zikiwa ni usafi, ufungaji wa vifaa tiba, ukaguzi wa mifumo ya maji na umeme pamoja na umaliziaji wa nje.

Jengo hilo lina uwezo wa kuhudumia watoto wachanga 42 kwa wakati mmoja, wakiwemo watoto njiti na wenye changamoto mbalimbali za kiafya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI IDARA YA MAAFA OWM AFUNGA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA DHARULA MWANZA

    February 20, 2026
  • KAYA 19,344 KUNUFAIKA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE MWANZA AWAMU YA KWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AMPOKEA WAZIRI DEUS SANGU MWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WASIMBE NA WABANZA KUUNGANA KUKATA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.