• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO NA KUFUNDISHIA VYENYE THAMANI YA ZAIDI YA MILIONI 36 MISUNGWI

Posted on: February 12th, 2025

RC MTANDA AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO NA KUFUNDISHIA VYENYE THAMANI YA ZAIDI YA MILIONI 36 MISUNGWI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo tarehe 12 Februari, 2025 amekabidhi vifaa vya kufundishia na michezo vyenye thamani ya zaidi ya Tshs. Milioni 36 kwa shule 3 za Sekondari Wilayani Misungwi vilivyototelewa na Taasisi ya Africa School House.

Akiongea mara baada ya kukabidhi msaada huo katika hafla iliyofanyika katika shule ya sekondari ya Aimee Milembe, Mhe. Mtanda amewashukuru wahisani hao kwa msaada huo muhimu kwa maendeleo ya sekta ya elimu Wilayani humo na Mkoa wa Mwanza kwa ujumla.

"Elimu ndio mtaji mkubwa katika maisha na tunaamini kwenye kuwekeza kwa watoto na katika kufanikisha hilo Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan inatoa fedha nyingi kwenye elimu na tunawashukuru washirika wetu kwa kuwa nasi tangu mwaka 2017 kwa kujenga shule sehemu mbalimbali, nyumba za walimu, visima virefu vha maji." RC Mtanda.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesema ndani ya miaka minne shule mpya 11 za sekondari zimejengwa, mabweni 30, nyumba 12, matundu vya vyoo 133 kwa sekondari na kwamba awali zilikuwepo shule 965 za msingi na sasa 1043 sawa na ongezeko la shule 85 na shule 275 hadi 332 za sekondari sawa na ongezeko la shule 57.

Mhe. Mtanda ameongeza kuwa ndani ya kipindi cha miaka 4 walimu 1168 wameajiriwa na kupangiwa vituo ndani ya Mkoa huo na kwamba Serikali imepata mafanikio kwa kuwa na miundombinu hivyo basi wahisani hao kuunga mkono juhudi hizo ni jambo la msingi sana.


Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Dkt. Aimee Bessire amesema wanayo furaha kusaidia sekta ya Elimu na siyo tu kwa vifaa hivyo bali wanajenga pia miundombinu kama mabweni, madarasa, vyoo na jiko wilayani humo vinavyogharimu zaidi ya Tshs. milioni 350.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.