• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AKUTANA NA VIONGOZI WA JUMUIYA YA MARIDHIANO KANDA YA ZIWA

Posted on: January 29th, 2025

RC MTANDA AKUTANA NA VIONGOZI WA JUMUIYA YA MARIDHIANO KANDA YA  ZIWA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda amekutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa Jumuiya ya maridhiano Kanda ya ziwa (JMAT) na kuwashukuru kwa kazi nzuri wanayoifanya na kusisitiza bila amani nchini hakuna maendeleo.

Akizungumza na uongozi huo kwenye ukumbi mdogo wa Ofisi ya mkuu wa mkoa leo Januari 29,2025,Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha viongozi hao wa dini waliopo katika ziara ya kutembelea miradi ya kimkakati, kuzidi kuhubiri mema yote yanayofanywa na Serikali na inapobidi kukosoa basi nafasi hiyo itumike kwa hekima na busara.


"Wapo baadhi ya watu wanaweza kuwabeza katika hayo majukumu yenu lakini nawasihi msirudi nyuma kwani siyo dhambi kuhubiri ukweli kinachofanywa na Serikali yetu,"Mkuu wa Mkoa.

Mhe.Mtanda amewapongeza viongozi hao kwa uamuzi wa kutembelea miradi ya kimkakati ikiwemo ujenzi wa Meli mpya ya Mv Mwanza na Daraja la JP Magufuli na kujionea lengo la Serikali la kuinua Mkoa wa Mwanza kiuchumi na kuongeza pato la Taifa

"Ndugu zangu hivi sasa tunachangia pato la Taifa asilimia 7 na baada ya miradi hii kukamilika tutafika asilimia 10 hadi 12 kutokana na mkoa wetu kuwa eneo la kimkakati Mataifa jirani yatakuja kwa wingi hapa kufanya biashara,"Mtanda.

Kiongozi wa msafara huo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Alhaj Mussa Kalukwenyi amesema wataendelea kushirikiana na Serikali kuhakikisha jamii inaishi kwa amani na ziara yao itazidi kuwaelimisha mipango mizuri ya kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Viongozi  hao ambao ni wenyeviti na makatibu wa mikoa, wanatokea mikoa ya Geita,Mara na Simiyu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAKUZI YA AWALI YA MTOTO MSINGI WA UJENZI WA TAIFA IMARA - RAS BALANDYA

    May 16, 2025
  • RC MTANDA AWAKARIBISHA MWANZA WANAFUNZI KUTOKA UGANDA

    May 15, 2025
  • RC MTANDA AKOSHWA NA BONANZA LA USHIRIKA NA MABENKI

    May 14, 2025
  • RAS MWANZA ATAKA UHAMASISHAJI CHAKULA CHENYE LISHE KUONGEZEKA SHULENI

    May 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.