• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AKUTANA NA WAKUU WA TAASISI, VIONGOZI WA WAFANYABIASHARA, AHIMIZA ULIPAJI KODI NA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

Posted on: May 9th, 2024

RC MTANDA AKUTANA NA WAKUU WA TAASISI, VIONGOZI WA WAFANYABIASHARA, AHIMIZA ULIPAJI KODI NA HUDUMA BORA KWA WANANCHI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Mei 9, 2024 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa amekutana kwa nyakati tofauti na Wakuu wa Taasisi za Umma, viongozi wa Wamachinga na viongozi wa Wafanyabiashara kwa lengo la kufahamiana na kufahamu shughuli zao.

Akianza mkutano huo na Wakuu wa Taasisi za Umma, Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha kutambua wajibu wao kwa kutoa huduma bora kwa wananchi na kwa wakati.

"Rais Samia ameonesha kwa vitendo anavyowapigania maendeleo wananchi,na sisi tunavyotoa huduma bora wananchi watazidi kuifurahia Serikali yao",Mkuu wa Mkoa

Amewataka viongozi hao kutekeleza wajibu wao kwa kuimarisha nidhamu ya utumishi wa umma kwa kufanya kazi kwa upendo na kuheshimiana na kuepuka aina yoyote ya unyanyasaji au kupokea rushwa kutoka kwa wananchi

Amesema yupo mbioni kuanza ziara kutembelea maeneo yote mkoani humo ili kujionea maendeleo ya wananchi na changamoto zinazowakabili.

"Ndugu viongozi mkutano huu siyo wa kusikiliza changamoto zenu na kuzitolea majibu hapa la hasha! lengo ni kufahamiana na kujua shughuli zenu mkitambua sina muda mrefu tangu nihamishiwe hapa nikitokea Mara,"amesema Mhe.Mtanda.

Katika mkutano wake wa pili na viongozi wa Wafanyabiashara wadogo maarufu kama Wamachinga,Mhe.Mtanda amewaahidi kuwatembelea maeneo yao ili kujionea hali halisi kabla ya kuchukua maamuzi yenye malengo ya kuboresha shughuli zao.

"Mkoa wa Mwanza una jumla ya masoko 50 yenye wafanyabiashara wadogo 19,969 ambao wapo katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza,"Yesaya Sikindeni,Afisa Biashara Mkoa.

"Nimesikia changamoto zenu uzuri nina uzoefu wa kutosha na kero zinazo wasumbua,nimesikia taarifa fupi kutoka kwa Afisa biashara ikiwemo hali ya masoko na mazingira yenu,kuweni na utulivu na fanyeni shughuli zenu kwa kuheshimu maelekezo mliyopewa na Serikali,"Mkuu wa Mkoa

Akimalizia mkutano huo na viongozi wa Wafanyabiashara wakubwa ,mkuu huyo wa Mkoa amebainisha anatambua mchango wao katika pato la Taifa na kusisitiza kuendelea kushirikiana katika ujenzi wa Taifa.

"Tujengeni nidhamu ya ulipaji kodi kwa uungwana na Serikali imeweka bayana masikilizano baina ya mamlaka za kodi na wafanyabiashara hakuna mtu wa kukufungia biashara yako," Mhe.Mtanda.

Amewakumbusha pia Mamlaka za usimamizi wa kodi kuwacha kutumia lugha za vitisho au aina yoyote ya utovu wa nidhamu badala yake kufanya kazi zao kwa kufuata Sheria na kanuni zilizopo huku wakiweka mazingira rafiki na wafanyabiashara.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.