Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AONGOZA MAPOKEZI YA WAZIRI WA FEDHA JIJINI MWANZA

Posted on: September 17th, 2024

RC MTANDA AONGOZA MAPOKEZI YA WAZIRI WA FEDHA JIJINI MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewaogoza Wakuu wa Idara, Sehemu na Vitengo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa katika mapokezi ya Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba aliyewasili Jijini Mwanza kwa ziara ya kikazi.

Akizungumza mara baada ya kumpokea Waziri huyo Mhe. Mtanda ameshukuru Mhe. Rais kupitia Wizara hiyo kwakuwa amekuwa akiidhinisha fedha nyingi za miradi mbalimbali inayotekelezwa Mkoani humo ikiwemo ile ya kimkakati kupitia Wizara ya Fedha.

"Ofisi yangu imekuwa ikipokea fedha nyingi sana, kipekee ninamshukuru sana Mhe. Rais ameendelea kutuletea fedha nyingi za miradi kupitia wizara yako, na sisi tunakuahidi Mhe. Waziri tutaendelea kuzisimamia fedha hizi ili zikatumike kama ilivyokusudiwa kwa lengo la kuwaletea wananchi wa Mwanza maendeleo". Amesema RC Mtanda.

Naye Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amesema ujio wake katika Mkoa wa Mwanza ni kuja kukagua, kuzindua na kutembelea miradi mbalimbali ambayo Serikali imekuwa ikiitekeleza katika Mkoa wa Mwanza na kuzungumza pia na wananchi kuwaleza namna serikali inavyoeendelea kuratibu na kutekeleza miradi hiyo.

Mhe. Dkt. Mwigulu amesema Mhe. Rais Dkt. Samia amekuwa akitoa fedha nyingi za miradi na ameendelea kukuhakikisha anatimiza ahadi yake ya kuwaletea maendelea wananchi wa Tanzania hivyo amedhamiria kutembelea na kukagua miradi yote kuanzia ngazi za juu mpaka za vitongoji ili kujionea ufanisi wa utekelezaji wa miradi hiyo.

"Nimeambatana pia na Wataalamu wangu kutoka Wizarani lakini pia kutoka maeneo mbalimbali ya kisekta ili kuhakikisha katika ziara hii pia tunatatua na kutoa elimu kuhusu masuala mbalimbali yakiwemo yale ya kimfumo kama vile NeST". Amesema Waziri wa Fedha.

Mhe. Dkt. Mwigulu aliwasili Mkoani Mwanza ijumaa ya tarehe 13 Septemba 2024 ambapo alianza ziara yake rasmi Wilayani Misungwi kwa kutembelea mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Mwanza na kisha kuzungumza na Wananchi wa Misugwi Mjini na leo ameendelea na ziara yake Wilayani Nyamagana ambapo atakagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Soko Kuu la Mjini Kati Jijini Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA YATOA SALAMU ZA PONGEZI KWA PROF.JANABI

    May 20, 2025
  • LENGO LA HOSPITALI ZA WILAYA NI KILA MWANANCHI APATE HUDUMA MAHALI ALIPO - WAZIRI MKUU

    May 19, 2025
  • MITAMBO YA KUOPOA MAGUGUMAJI KUWASILI MWISHONI MWA MWEZI JULAI.

    May 19, 2025
  • WAZIRI MKUU AWATAKA WANAMALYA KUCHANGAMKIA FURSA YA CHUO CHA MICHEZO

    May 18, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.