• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA MTOTO WA KATIBU WAKE

Posted on: November 16th, 2024

RC MTANDA AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA MTOTO WA KATIBU WAKE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Novemba 16, 2024 amewaongoza watumishi wa Ofisi yake na waombolezaji katika mazishi ya mtoto wa katibu wake Faith Matia Levi.

Akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya Mkuu wa mkoa kwenye Kanisa la KKKT Usharika wa Imani, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe.Christopher Ngubiagai  amewataka familia ya Bw.Matia Levi kusimamia imara na kumtumainia Mwenyezi Mungu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na kipenzi chao.

Amesema siku zote kifo huwa hakizoeleki na kinakuja pasipo kutarajia hivyo wanapaswa kumshukuru Mungu kwa kila jambo.

"Nawashukuru wote tulioguswa na msiba huu tangu taarifa ilipotolewa na kuwafariji wafiwa, tuendelee kuwatia nguvu na moyo wafiwa katika muda huu wa maombolezo", DC Ngubiagai.

Awali akitoa mahubiri wakati wa ibada ya mazishi mchungaji wa kanisa hilo amesema mwanadamu hana sababu ya kuwa na hofu ya kifo kwani siku yake ya kurejea kwa Mungu ipo hivyo wajibu wake ni kuishi kwa furaha kwa kumtumainia Mungu.

"Leo wafiwa wana huzuni ya kumpoteza mtoto wao, lakini hili ni fumbo kwa Mungu la kumtwaa Faith akiwa na umri mdogo ili akapate nafasi zaidi ya kutuombea na sisi tunaondelea na zawadi hii ya uhai", Mchungaji Mahisa.

Akitoa historia fupi ya marehemu, mama mdogo wa marehemu amesema Faith alizaliwa Februari

06, 2019 hospitali ya Kanda ya Bugando akiwa ni mtoto wa tatu kuzaliwa ambaye hadi mauti yanamkuta hospitali ya Mkoa ya rufaa ya Sekou Toure Novemba 13, a024 alikuwa darasa la awali shule ya msingi Nyakahoja huku akiwa na ndoto za kuwa daktari wa hospitali ya Sekou Toure.

Salamu mbalimbali za rambi rambi zimetolewa kwa wafiwa ikiwemo Ofisi binafsi ya Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa, Taasisi za Umma,Taasisi za dini, umoja wa wabunge Mkoa wa Mwanza na makundi mengine mbalimbali yanayoshirikiana na Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza

Marehemu Faith Matia amepumzishwa kwenye nyumba yake ya milele alasiri ya Novemba 16, 2024 Kisesa wilayani Magu ambako ni eneo la familia.

Bwana ametoa Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.