• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ASHUHUDIA SAFARI YA KWANZA YA MV NEW MWANZA KWENDA BUKOBA

Posted on: September 21st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo tarehe 21 Septemba, 2025 ameshuhudia jaribio la mwisho la safari ndefu kwa Meli ya MV New Mwanza kwenye bandari ya Mwanza Kusini iliyopo jijini Mwanza ilipoondoka kuelekea kwenye Bandari ya Bukoba (Neutical Miles 100).

Akizungumza na wananchi waliojitokeza kushuhudia hafla hiyo ya kihistoria Mhe. Mtanda amesema kukamilika kwa meli hiyo ni ishara ya juhudi za serikali katika kuimarisha sekta ya usafiri na usafirishaji wa abiria na mizigo katika ukanda wa ziwa Victoria.

Aidha, amesema wananchi wa Mwanza na ukanda wa ziwa Victoria kwa ujumla wamepata usafiri wa uhakika kwani Mhe. Rais Samia amedhamiria kuwaondoka kwenye adha ya ajali zilizotokana na matumizi ya usafiri duni wa mitumbwi na kwamba nauli zitakua nafuu sana kwa safari za ndani na nje ya nchi.

Ameongeza kuwa katika kuhakikisha katika ukanda huo kunakua na usalama katika usafiri, usafirishaji na hata uvuvi serikali kwa kushirikiana na nchi wanachama wa Jumuiya Afrika Mashariki wanajenga kituo maalum cha uokozi katika eneo la Malaika Beach kwa gharama ya zaidi ya Bilioni 5.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Meli nchini (TASHICO) Bw. Eric Hamissi amebainisha kuwa Ujenzi wa meli hiyo umefikia asilimia 99 na baada ya safari hiyo ya Mwanza- Kemondo hadi Bukoba wanatarajia kupata majibu ya ufanisi wake kitaalamu na mara moja kuanza safari katika Ziwa Victoria.

Amesema, pamoja na changamoto kama za kupanda kwa gharama za vifaa kama vya vyuma na wataalamu kushindwa kufika kwa wakati hatimaye meli hiyo ya kisasa yenye urefu wa mita 92.6 yenye spidi kubwa leo hii imekamilika na itafika Bandari ya Bukoba kwa saa 6 pekee.

Aidha, amebainisha kuwa meli hiyo yenye uzito wa tani elfu nne (4000) na ghorofa nne, ina uwezo wa kubeba abiria 1200, Magari 20 madogo, Malori 3 imejengwa na watanzania zaidi ya 200 walioshirikiana na timu ya wataalamu 16 tu  wa mkandarasi kutokea nchini Korea Kusini.

"Kwa mara ya kwanza Meli hii itafika katika bandari ya Bukoba na italala huko na kesho itarejea Mwanza na imejengwa kwa zaidi ya Tshs. Bilioni 120 ambapo ni lazima tumshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani ameikuta kwenye 40% tu ya ujenzi mwaka 2021 huku zikiwa zimelipwa Tshs. Bilioni 36 pekee lakini amemalizia fedha zote." Amebainisha Mkurugenzi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA ATOA UFAFANUZI JUU YA CHANGAMOTO YA MAJI

    September 23, 2025
  • HUDUMA ZA MSAADA WA KISHERIA KUTOLEWA KWENYE MAGEREZA MWANZA

    September 22, 2025
  • RAS BALANDYA ATOA WITO KWA JESHI LA POLISI KULINDA AMANI KATIKA UCHAGUZI MKUU

    September 22, 2025
  • RC MTANDA ASHUHUDIA SAFARI YA KWANZA YA MV NEW MWANZA KWENDA BUKOBA

    September 21, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.