• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATAKA KANUNI ZA KILIMO BORA ZAO LA PAMBA ILI KUONGEZA UZALISHAJI

Posted on: November 18th, 2024

RC MTANDA ATAKA KANUNI ZA KILIMO BORA ZAO LA PAMBA ILI KUONGEZA UZALISHAJI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wakulima wa pamba mkoani humo kung'oa na kuchoma moto mazalia ya Pamba ya msimu uliopita kabla ya Septemba 15 ya kila mwaka ili kutoathiri msimu mpya wa kilimo hicho.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo mapema leo Jumatat  Novemba 18, 2024 wakati akifunga kikao cha viongozi ngazi ya wilaya kwa ajili ya kampeni ya ung'oaji wa masalia ya Pamba wilayani Kwimba.

Amesema kutofanya hivyo kunasababisha wadudu kuzaliana na kusubiri pamba mpya shambani kuiharibu, hivyo ili kujihakikishia uzalishaji wenye tija ni lazima wakulima wafuate kanuni za kilimo cha zao hilo kwa kusafisha mashamba mapema kabla ya msimu mwingine.

"Viongozi wote mpo hapa maafisa ugani, tarafa, kata na vijiji nawaagiza  muda wa hiyari umekwisha twendeni tukatekelze kanuni bora za kilimo cha Pamba kwani zao hili ndio injini ya uchumi wa wananchi wa Mwanza kwa miaka mingi." Mtanda.

Aidha, ameipongeza bodi na kwa kipekee balozi wa Pamba nchini,Aggrey Mwanri kwa juhudi zake za uelimishaji wakulima wa Pamba nchini na kwa kipekee mkoani Mwanza ambako kimsingi amechagiza uzalishaji na kufanya idadi ya wakulima waliopo mkoani humo kuwa sawa na waliopo kwenye mikoa 17 nchini.

Balozi wa Pamba Mhe. Agrey Mwanri amesema tatizo kubwa linalokwamisha Mbegu mpya kumea kwenye mashamba ya Pamba ni wakulima kutong'oa maotea ya pamba ya msimu uliopita kwani msimu mpya unachelewa na hatimaye mvua za vuli zinawapita.

Amefafanua kuwa mwisho wa kusafisha pamba ni tarehe 15 Septemba, 2024 ya kila mwaka ili msimu mpya uanze lakini wapo baadhi ya wakulima wamekua wakiacha maotea kwa lengo la kulisha mifugo kinyume na kanuni za kilimo bora na kupelekea kukwamisha uzalishaji.

"Mkiruhusu mimea ya msimu uliopita kuendelea kubaki shambani mtakua mnakaribisha wadudu kama Chawajani, Kandambili na ndio maana hivi sasa neema na baraka ya zao la pamba kwenye uchumi wa wananchi zimepungua kutokana na kushuka kwa takwimu za uzalishaji."  Mwanri.

Aidha, amekemea tabia ya wakulima kuchanganya mazao na akatoa mfano wa Pamba na Mahindi yakioteshwa kwenye shamba moja yanasababisha zao moja kushiba rutuba na kulikwamisha jingine na kwakua Mahindi yanamea kwa haraka basi pamba itaathirika.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.