• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATOA SIKU 10 KUKAMILISHWA UJENZI WA SEKONDARI YA NELA, KWIMBA

Posted on: January 16th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amempa mkandarasi anayejenga Shule ya Sekondari Nela wilayani Kwimba siku 10 kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya madarasa nane pamoja na matundu 16 ya vyoo ili kuwezesha wanafunzi kuanza masomo.

Agizo hilo limetolewa mapema leo Januari 16, 2026 wakati Mhe. Mtanda alipokuwa katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika Kijiji cha Nela ambapo alikagua ujenzi wa shule hiyo unaotekelezwa kwa gharama ya shilingi milioni 267.050 na Mkandarasi wa Kampuni ya Mairo Group of Companies, na kubaini kuwepo kwa ucheleweshaji wa utekelezaji wa mradi.

Katika kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati Mhe. Mtanda amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba kufanya tathmini ya kazi zote zilizotekelezwa hadi sasa na kuhakikisha anampatia mzabuni mwenye uwezo wa kukamilisha ujenzi uliobaki kwa kutumia fedha ambazo bado mkandarasi wa awali hajalipwa.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesisitiza umuhimu wa kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo kwa kufanya kazi usiku na mchana akibainisha kuwa tarehe ya Februari 28, 2026 ambayo awali ilipangwa kuwa mwisho wa mradi ni mbali na inaweza kuwanyima wanafunzi fursa ya kuanza masomo kwa wakati.

Halikadhalika, Mhe. Mtanda ameagiza Ofisi ya TAKUKURU wilayani Kwimba kufuatilia kwa kina mwenendo wa zabuni ya ujenzi wa shule hiyo pamoja na utendaji wa Idara ya Manunuzi kwa ujumla na kuwasilisha taarifa ya uchunguzi huo.

Wakati huo huo, Katibu Tawala wa Mkoa ameagizwa kumwondoa Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi katika halmashauri hiyo na kumhamishia mkoani kufuatia tuhuma za uzembe na ukiukwaji wa taratibu za manunuzi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU AZINDUA MELI MPYA YA MV NEW MWANZA, ATOA MAAGIZO KWA MIRADI ILIYOSIMAMA

    January 23, 2026
  • WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI SAHWA -MWANZA

    January 23, 2026
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA INAJALI MAISHA YA WANANCHI WAKE - WAZIRI MKUU

    January 23, 2026
  • WAZIRI MKUU ATUA MWANZA KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU MOJA

    January 23, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.