• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA SHIMIWI KUTATUA MIGOGORO KUPITIA VIKAO

Posted on: September 16th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka Sekretarieti ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) kutatua migogoro yao kupitia vikao ili kuboresha zaidi mashindano hayo.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo Septemba 16, 2025 katika uwanja wa Mpira wa CCM Kirumba wilayani Ilemela alipokua akifunga rasmi mashindayo hayo mwaka 2025 yaliyodumu kwa takribani siku 16 za mitanange kupitia michezo mbalimbali.

Amesema, wanapohitimisha michezo hiyo wahakikishe wanaketi pamoja na kushughulikia mapungufu yaliyojitokeza na kuyatatua ili kwenye michuano ijayo kuwe na ufanisi zaidi badala ya kukutana wakiwa na migogoro ambayo huathiri michezo.

Aidha, amewataka watumishi mbalimbali kujisajiri kwenye mfumo rasmi wa wanamichezo chini ya usimamizi wa sekretarieti ya SHIMIWI ili kuwa na kanzifata maalumu ya wanamishezo na kuweza kuhuisha kila wakati vinapotokea vipaji.

Vilevile, ametoa wito kwa shirikisho hilo kuhakikisha wanahusisha watu wenye ulemavu ambao wapo kwenye utumishi wa umma kwa mujibu wa sheria na kushirkiana na wizara mama ya michezo katika kulinda na kuboresha miundombinu ya michezo.

Kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Savera Slavatory ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu wa wizara hiyo amesema wanamichezo 3165 wameshiriki mashindano hayo kutoka kwenye vilabu 65 kwa muda wa siku 16 kwa mafanikio makubwa.

Aidha, ameahidi kuwa wizara hiyo itasimamia haki wakati wote kwa kuhakikisha sheria zinafuatwa na ameitaka sekretarieti ya SHIMIWI kurekebisha makosa madogo yaliyojitokeza kwa ajili ya kujifunza kwa michuano ijayo na akatoa rai kwa waajiri kuhakikisha wanapeleka watumishi kwenye michuano hiyo.

Awali uwanjani hapo, Mkuu wa Mkoa ameshuhudia fainali kwa michezo ya kuvuta Kamba ambapo Ofisi ya RAS Tanga wamewabwaga TAKUKURU kwa Wanawake huku OR- IKULU wamewapiga TAKUKURU wanaume. Na Mshindi wa jumla SHIMIWI 2025 ni TAKUKURU.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AWATAKA SHIMIWI KUTATUA MIGOGORO KUPITIA VIKAO

    September 16, 2025
  • WAHALIFU NA WANYANG’ANYI ZIWA VICTORIA KUTAFUTA SHUGHULI NYINGINE ZA KUFANYA

    September 16, 2025
  • RC MTANDA ASHUHUDIA USHUSHAJI WA VIVUKO MAJINI, WANANCHI VISIWANI MKAO WA KULA

    September 16, 2025
  • RC MTANDA AWAALIKA WALIOKOSA ELIMU RASMI KUJIUNGA NA MPANGO WA ELIMU WATU WAZIMA

    September 15, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.