• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA WAKANDARASI WA UMEME MWANZA KUFANYA KAZI KWA UADILIFU

Posted on: February 2nd, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amepokea rasmi utambulisho wa wakandarasi wapya wa kupeleka umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya Mkoa wa Mwanza chini ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kipindi cha miaka mitatu.

Wakandarasi hao ni White City International Contractors Ltd na Tibea Company Ltd, ambao wamesaini mikataba miwili ya utekelezaji wa mradi huo mkubwa unaolenga kusogeza huduma ya umeme kwa wananchi wa vijijini na maeneo ya pembezoni.

Akizungumza wakati wa utambulisho huo, Mhe. Mtanda amewataka wakandarasi hao kufanya kazi kwa weledi, uaminifu na kuzingatia maadili ya kazi ili kufanikisha malengo ya Serikali ya kuwahudumia wananchi kwa haki na usawa.

Amesema Ofisi yake itafanya ukaguzi wa mara kwa mara kufuatilia utekelezaji wa mradi huo, huku akisisitiza kuepuka vitendo vya rushwa wakati wa kuwaunganisha wananchi na huduma ya umeme.

Mhe. Mtanda pia ametoa wito kwa wananchi kuwapokea vizuri wakandarasi hao na kuhakikisha wanapitia ngazi zote za Uongozi kuanzia Wilaya, Kata, Kijiji hadi Kitongoji ili kuwaelezea Viongozi kwa kina kuhusu mradi huo na vigezo vya uunganishaji.

Ameeleza kuwa nia ya Serikali ni kusogeza huduma karibu na wananchi, na pale mahitaji yatakapoongezeka, maboresho yatafanyika ili kuongeza upatikanaji wa umeme kwa wananchi wengi zaidi.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Miradi kutoka Ofisi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Seif Abdallah amesema Mkoa wa Mwanza umesaini jumla ya kandarasi mbili kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.

Amesema mradi huo utatekelezwa katika vitongoji 619 vya wilaya tano za Mkoa wa Mwanza kwa gharama ya shilingi bilioni 66.7 na unatarajiwa kuwanufaisha wateja 19,878.

Amefafanua kuwa White City International Contractors Ltd itahudumia vitongoji 306 katika Wilaya za Misungwi na Magu kwa gharama ya shilingi bilioni 32.7, huku Tibea Company Ltd ikitekeleza mradi katika vitongoji 313 vya Wilaya za Kwimba na Sengerema kwa gharama ya shilingi bilioni 33.7.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AWATAKA WAKANDARASI WA UMEME MWANZA KUFANYA KAZI KWA UADILIFU

    February 02, 2026
  • MADIWANI MWANZA WAJENGEWA UWEZO UONGOZI NA USIMAMIZI WA MAENDELEO

    February 02, 2026
  • SERIKALI NA MCHANGO WAKE KATIKA USTAWI WA MAHAKAMA, MAENDELEO YA TAIFA NA UPATIKANAJI WA HAKI

    February 02, 2026
  • RMO MWANZA AZINDUA KAMBI YA UPIMAJI AFYA KWA WANANCHI

    January 31, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.