• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA WASIMBE NA WABANZA KUUNGANA KUKATA BIMA YA AFYA KWA WOTE

Posted on: February 20th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wananchi wa mkoa huo kuchangamkia fursa ya Bima ya Afya kwa Wote kwa kuunda kaya za watu sita ili kunufaika na huduma hiyo. Amewahimiza hata wanawake wasio na waume (wasimbe) na wanaume wasio na wake (wabanza) kuungana na kuunda kaya zitakazowawezesha kukata bima.

Mtanda amesema lengo ni kuondoa hofu kwa watu wasio na familia au waliotengana na wenza wao, kuwa nao wanaweza kujiunga kwa kushirikiana na wengine. Amesisitiza kuwa mpango huo ni wa wote na unalenga kuhakikisha hakuna mwananchi anayekosa huduma za afya kwa sababu ya ukosefu wa kaya rasmi.

Akizungumza katika Kijiji cha Mwanekeyi, Kata ya Matare, Wilaya ya Kwimba wakati wa uzinduzi wa Shule ya Msingi Mwanekeyi, RC Mtanda pia amewataka wazazi kuhakikisha wanawapeleka watoto wote wanaostahili kujiunga na elimu ya awali, msingi na kidato cha kwanza.

Amesema hadi sasa wanafunzi 6,622 wa kidato cha kwanza wameripoti shule Wilayani Kwimba, huku 1,587 bado hawajaripoti. Amewaagiza Mkuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama, Mkurugenzi na Maafisa Elimu kutembea nyumba kwa nyumba kuwatafuta watoto hao na kuwapeleka shule haraka.

Aidha, amesisitiza kuwa hakuna mwanafunzi anayepaswa kurudishwa nyumbani kwa kukosa sare, viatu au michango. Ameagiza watoto wapokelewe kama walivyo huku wazazi wakipewa muda wa kukamilisha mahitaji hayo, akionya kuwa kutotekeleza agizo hilo ni ukaidi.

RC Mtanda pia amewataka walimu na wanafunzi kuitunza miundombinu ya shule ili idumu kwa muda mrefu. Mradi wa ujenzi wa shule hiyo ulitekelezwa kwa siku 90 kuanzia Novemba 13, 2025 hadi Februari 9, 2026 kwa gharama ya Sh.330,700,000, ambapo Sh.300,684,969.06 zimetumika na Sh.30,015,030.94 zinaendelea kutumika kukamilisha kazi zilizobaki.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI IDARA YA MAAFA OWM AFUNGA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA DHARULA MWANZA

    February 20, 2026
  • KAYA 19,344 KUNUFAIKA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE MWANZA AWAMU YA KWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AMPOKEA WAZIRI DEUS SANGU MWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WASIMBE NA WABANZA KUUNGANA KUKATA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.