• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AZINDUA MRADI WA MAJI KABILA, WANANCHI ZAIDI YA 11, 000 KUNUFAIKA

Posted on: June 13th, 2024

RC MTANDA AZINDUA MRADI WA MAJI KABILA, WANANCHI ZAIDI YA 11, 000 KUNUFAIKA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Juni 13, 2024 amezindua mradi wa maji wenye thamani ya zaidi ya  Tshs. Milioni 205 uliojengwa kwa ushirikiano baina ya SBL na RUWASA unaotarajiwa kunufaisha zaidi ya watu 11000 kutoka kwenye vijiji vya N'gwamagoli na Kabila.

Akizungumza na wananchi baada ya kuzindua mradi huo Mhe. Mtanda ameishukuru Kampuni ya Serengeti Breweries na AFRIcai kwa kutoa Tshs. 180,274,000 na kushirikiana na RUWASA (zaidi ya Bilioni 25) waliotekeleza mradi uliohusisha vituo vya kuchotea maji 13, mtandao wa mabomba KM 6.3 pamoja na tangi la lita 90,000.

"Mkoa wa Mwanza umetenga jumla ya Tshs. 146,315,299,905 katika mwaka 2023/24 - 2024/25 ambapo Wilaya ya Magu pekee imetengewa jumla ya Tshs. 17, 017,927,019 ili kukamilisha miradi 7 inayoendelea kutekelezwa." Amesema, Mkuu wa Mkoa.

RC Mtanda amefafanua kuwa ujenzi wa mradi huo muhimu kwa wananchi ni utekelezaji wa agenda ya Rais Samia katika kusudio lake la kumtua mama ndoo kichwani na utelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020-2025 inayoitaka Serikali kufikisha huduma ya maji vijijini kwa 85% au zaidi hadi kufikia 2025.

"Serengeti Broweries Limited imetumia zaidi ya Tshs. Bilioni 2.5 2023/24 kwenye uchangiaji wa miradi ya huduma kwa jamii ikiwa ni katika kuhakikisha inasaidia kuondoa adha ya upatikanaji wa maji safi na salama na kupambana na ukame unaotokana na mabadiliko ya tabia nchi hususani vijijini." Mkurugenzi Mtendaji SBL, Dkt. Obinna Anyalebechi.

Mkuu wa wilaya hiyo Mhe. Joshua Nathari amewataka wananchi kulinda miundombinu ya mradi huo ili lengo la kuongeza upatikanaji maji pamoja na kupunguza umbali na muda wa kufuata maji lidumu kwa muda mrefu na kusaidia kumaliza kero ya maji moja kwa moja.

Naye Meneja wa Wakala ya Maji vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mwanza Mhandisi Godfrey Sanga amesema Januari 2024 ujenzi wa mradi ulianza na Aprili 2024 umekamilika na kuna matarajio ya kufikisha asilimia 86 kutoka 71 za usambazaji maji vijijini kwa wananchi wa wilaya ya Magu.

"Tulikua tunasumbuka sana na huduma za maji lakini kwa sasa usumbufu wote umeisha kutokana na Rais Samia kutupendelea maana kwenye vitongoji vyetu vitano kati ya sita sasa tumepata naji safi tunaomba mtupelekee huduma hii kwenye kijiji hicho cha Ilambu." Mwenyekiti wa Kijiji cha Kabila, Mwajibu Boniface.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.