• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA WATAKA WAZEE KUWA MABALOZI WA MAADILI MEMA

Posted on: June 7th, 2024

RC MTANDA WATAKA WAZEE KUWA MABALOZI WA MAADILI MEMA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wazee kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuelimisha vijana kuwa na Maadili mema na kuachana na tabia hasi zinazosababisha kuwepo na mmomonyoko wa maadili.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo wilayani Misungwi wakati akizungumza na wazee wa wilaya hiyo ambao kwa kauli moja wameonesha imani kubwa kwa Rais Samia katika kuliletea Taifa maendeleo.

"Ni lazima tujenge familia bora na imara, tunapaswa kujiandaa na kustaafu mapema na siyo kuongeza mke bali tunapaswa kujiandaa na uzee kwa kujiandalia mahali pa kuishi." Mhe. Mtanda.

Amebainisha kuwa fidia zinazolipwa kwa wananchi wa Fela wanaopisha mradi wa SGR ni ishara ya hatua kubwa zaidi ya maendeleo inayokuja kwa wananchi wa

Misungwi hivyo ni lazima kujiandaa kunufaika nazo kwa kuwekeza.

"Mradi wa kimkakati wenye thamani ya zaidi ya Bilioni 700 (Daraja la Kigongo Busisi) unakaribia kukamilika, ndani ya miezi 3 daraja letu linakamilika na kupitia takwimu za abiria wanaotumia kivuko inaonesha kuna watu wengi sana wanatumia barabara hiyo, tujiandae kunufaika," Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Vilevile, ameutaja mradi wa Ujazilizi wa Umeme wenye thamani ya zaidi ya Bilioni 8 na kuna megawati za umeme zaidi ya 80 lakini unaotumika ni umeme kidogo tu na kwamba zaidi ya Bilioni 11 zimekuja kusambaza umeme vijijini kupitia Wakala wa Umeme (REA).

"Serikali inasisitiza malezi bora ya watoto kuanzia unyonyeshaji hadi makuzi na kuwapatia elimu bora ili baadaye waweze kuwatunza wazee wao na Serikali inawahakikishia usalama popote walipo hata walio kwenye vituo vya malezi maalum na wanufaika wa mradi wa uhaulishaji fedha chini ya TASAF wataendelea kunufaika kwa mujibu wa taratibu." Mtanda.

Mkuu wa Wilaya ya Misungi Mhe. Johari Samizi amesema tatizo la maji kwenye kata ya Usagara linakwenda kumalizika hivi karibuni kwani tayari kuna mkandarasi anayejenga mradi wa maji mkubwa kwenye kata hiyo yenye vijiji vinne na akatoa agizo kwa watumishi wa afya kuwajali wazee bila kuchoka.

Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wilaya ya Misungwi Josiah Gambishi amesema anajivunia umoja na ushirikiano walionao ndani ya wilaya hiyo unaochagizwa na uongozi bora wa Mkuu wa Wilaya hiyo na kwa kauli moja wameonesha imani kwa uongozi wa Rais Samia na kusema anatosha kuongoza nchi kwa miaka 5 mingine.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.