• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mwanza aagiza Halmashauri zote kutenga na kupeleka fedha za Miradi ya Lishe kwa wakati

Posted on: June 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe, Mhandisi Robert Gabriel ameziagiza Halmashauri mkoani humo kutenga na kupeleka fedha za miradi ya Lishe kwa wakati ili kutekeleza Afua za Lishe na kuweza kusaidia jamii kuwa na afya bora na kuondoa Udumavu kwa watoto.


Mhandisi Robert Gabriel amesema hayo leo Juni 13, 2022 wakati akifungua kikao cha kupitia utekelezaji wa mkataba wa lishe, kupata taarifa ya Kampeni ya Chanjo ya Polio na Maandalizi ya kampeni ya Chanjo ya Uviko 19 kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Aidha, amewataka Maafisa Lishe kutoa taarifa ya utekelezaji wa zoezi la Afua za Lishe kwenye ofisi za Wakuu wa Wilaya kila wiki zikionesha mafanikio na changamoto  kwenye wiki husika ili kwa kushirikiana na Halmashauri waweze kufanikisha kampeni hiyo.


Kuhusu utekelezaji wa kampeni ya Chanjo ya Ugonjwa wa Polio Mhe Mkuu wa Mkoa amewapongeza wadau na viongozi kwa kufanikisha Chanjo hiyo kwa watoto zoezi ambalo yeye mwenyewe ndiye alizindua rasmi wilayani Ukerewe.

Vilevile, Chanjo ya Uviko 19 imeonesha Ukerewe kuongoza kwa idadi ya watu waliochanjwa hadi sasa kwa zaidi ya asilimia 65 na ndipo Mkuu wa Mkoa aliwapongeza na akatoa wito kwa Halmashauri ya Misungwi kuongeza nguvu kwenye zoezi hilo kwani wana asilimia 27 tu.

"Ni kweli kwamba utekelezaji wa Afua za lishe hauendi vizuri kutokana na fedha kutoelekezwa kwenye eneo hilo ila nakuhakikishia Mhe Mkuu wa Mkoa kwenye bajeti mpya ya mwaka wa fedha ujao tutahakikisha shughuli zote za lishe zinakwenda vizuri." Mganga Mkuu wa Mkoa, Dktr Thomas Rutachunzibwa.

Baadae iliwasilishwa taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa Hospitali za Halmashauri huku Ilemela wakifikia asilimia 95 hatua ya umaliziaji kwa asilimia 95 huku Misungwi wakifikia asilimia 47 pamoja na Kwimba ambao amewataka kuharakisha ujenzi bila kusahau mifumo ya TEHAMA hadi kufikia Juni 30, 2022.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.