• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

REA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MWANZA, KILA WILAYA KUPATIWA MITUNGI YA GESI 3,255

Posted on: December 2nd, 2024

REA KUSAMBAZA MITUNGI YA GESI 19,530 MWANZA, KILA WILAYA KUPATIWA  MITUNGI YA GESI 3,255


Wakala wa Nishati ya Umeme Vijijini (REA) unatarajia kusambaza majiko ya gesi ya kilo sita 19,530 kwa bei ya ruzuku (Nusu bei) katika Mkoa wa Mwanza kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa tarehe 02 Disemba 2024 katika Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, kila Wilaya itapokea mitungi 3,255 ambayo itauzwa kwa shilingi elfu 20 badala ya shilingi elfu 40, huku nusu nyingine ya gharama ikigharamiwa na serikali kupitia ruzuku.

Akizungumza wakati wa kutambulisha mradi Mhandisi Mwandamizi wa Wakala wa nishati Vijijini (REA), Deusdedith Malulu amesema Serikali itagharamia shilingi bilioni 8.6 ikiwa na azma ya kufikia malengo ya Serikali ya matumizi ya 80% ya nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Aidha Mhandisi Malulu amesema mradi mwingine utakaogharamiwa na Serikali ni mradi wa usambazaji wa nishati ya umeme wa jua (Solar) ambapo nishati hiyo itauzwa kwa bei ya ruzuku ya 75% ambapo wanufaika ni wananchi waishio Visiwani na watapata nishati hiyo kwa shilingi laki moja hadi mbili badala ya makadirio ya shilingi laki 6.


"Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kufikisha nishati ya umeme katika maeneo yote nchini na kwa kutambua hilo imeona adha wanayoipata wananchi wa Visiwani na kuamua kuwaletea nishati ya umeme wa jua ambazo watazipata kwa punguzo la 75%".


Kadhalika mradi wa tatu ambao umetambulishwa ni mradi wa utoaji wa mikopo yenye masharti na riba nafuu iliyolenga kuwawezesha wananchi kujenga vituo vidogo vidogo vya mafuta maeneo y vijijini ili kurahisisha huduma ya upatikanaji wa mafuta maeneo ya vijijni.


"Kiasi ambacho tunatarajia kukopesha ni kuanzia shilingi milioni 133 kwa masharti nafuu kabisa na waombaji wote wanashauriwa kutembelea tovuti yetu ya www.rea.go.tz na watakutana na bango linalojieleza". Ameongeza Mhandisi Malulu.

Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa ya miradi hiyo Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Mhandisi Chagu Nghoma ameishukuru REA na serikali kwa ujumla kwa kutoa ruzuku katika nishati hizo muhimu (Umeme wa Jua, majiko ya gesi pamoja na mikopo nafuu ujenzi wa Vitu vya mafuta vijijini) na kuwataka wananchi kuchangamkia fursa hiyo adhimu.

"Sisi kama Mkoa tutahakikisha tunatoa elimu ya kutosha kwa wananchi juu ya umuhimu na matumizi ya nishati safi na kuwahamasisha pia wachangamkie fursa hii ambayo Mhe. Rais amedhamiria kuwainua wananchi waishio Vijijini". Amesema Mhandisi Chagu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.