• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali imepongezwa kuwatunza wenye Ualbino

Posted on: June 25th, 2019

 Serikali  imepongezwa na Shirika la Under The Same Sun kwa namna ilivyoshiriki kupunguza   mauaji na ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi tangu 2008 hadi 2018 ambapo matukio yamepungua kutoka 40 kwa mwaka na kufikia nane.

Shirika hilo limesema licha ya mauaji kupungua kwa asilimia 90 bado kundi hilo linakumbwa na vitendo vya  unyanyapaa na kutopewa nafasi ya ajira   ambapo jamii imekuwa ikiwaita majina mbalimbali ya kebehi yakiwamo ya wanyama.

Akizugumza na waandishi wa habari jana katika kambi ya wiki moja iliyowekwa katika Chuo cha Walimu Butimba jijini Mwanza iliyopewa jina la ‘Summer Camp 2019’, Muasisi wa Shirika hilo kutoka Canada, Peter Ash alisema   ni mafanikio makubwa kwa shirika na Serikali kufikia hatua ya albino kuisha bila hofu.

“ Mauaji  au matukuo yamepungua sana, mfano tangu mwaka 2008  matukio yalikuwa 40 kwa mwaka lakini yameendelea kupungua hadi kufikia  nane mwaka jana, mpaka tunavyozungumza sasa kwa mwaka huu wa 2019, matukio yameripotiwa mawili tu.

“Jambo ambalo badi linaonekana linaendelea ni unyanyapaa na kutopatiwa fursa ya ajira, wapo watu wanawaita majina ya wanyama kama mbuzi, nguruwe na majina mengine ya kikabila suala hili tunaendelea kutoa elimu kwa jamii, pia vitendo vya baba kutelekeza familia kutokana na mama kujifungua mtoto mwenye ulemavu wa ngozi vimepungua na sasa wanawalea.

“Hapo awali kulikuwa na mtazamo kwamba watu wenye ualbino hawafariki bali wanapotea tu, vile vile mitazamo ya jamii ilikuwa kwamba ukimgusa  ni kosa  hivyo hivyo ilionekakana mama akijifungua  mtoto wa namna hiyo ni mkosi lakini leo wanashirikiana kwa kula na kulala pamoja, jambo ambalo tunalisisitiza kupewa ajira, inaweza kutokea kuna nafasi lakini ni ngumu kupewa licha ya kuwa na vigezo,”alisema.

Ash alisema  alisema shirika hili liliamua kuja Tanzania kutokana na  vitendo vilivyokuwa vikifanyika  vya ukataji viugo vya albino kutokana na imani za kishirikiana ambapo kutokana na jitihada walizozifanya za utoaji elimu kwa jamii, wanajisikia faraja kuona uahueni imepatikana.

Aliongeza kuwa mpaka sasa kuna watu wenye ualbino 400 wanaolelewa na shirika hilo  ambapo wale wanaosoma wanalipiwa ada, vifaa vya shule na kuwakatia kadi za afya kutoka   Mfuko wa Taifa wa Afya (NIHF) huku akiwataka jamii kuelewa kuwa ualbino ni hali ya kawaida   ya kurithi inayotoka kwa baba na mama.

Ash alisema kwa kipindi  cha miaka 10 sasa amegundua kwmaba watu wenye ulemavu wa ngozi wana akili kubwa na ujuzi  hivyo aliiomba Serikali  na mashirika binafsi inapotokea fursa ya ajira kundi hilo litazamwe ili waweze kuwa sehemu ya viongozi.

Naye Mkurugenzi wa  Shirika la Under The Same Sun-Tanzania, Berthasia Ladislaus kambi hiyo  yenye watoto 180 kutoka mikoa yote Tanzania bara watakuwepo hapo  kwa lengo la kujifunza mambilimbali na kuonyesha vipaji.


“Watoto hawa wametoka mikoa yote na tumechukua 180 ingawa shirika linalea 400, hapa watafundishwa mambi mengi na kuonyesha vipaji, tumekuja hapa na wachungaji, watalaamu wa mambo mbalimbali wakiwamo wabebezi wa uandishi wa habari ili nao watoe elimu maana wapo watoto wanaopenda kuwa waandishi.

“Jambo ambalo tunasisitiza kwa jamii, mashirika ya binafsi na Serikali ni kwamba tunao vijana waliofikia vyuo vikuu na wanafanya vizuri sana, hivyo wapewa fura inapojitokeza  ili na wao wawe viongozi katika ngazi za juu,”alisema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.