• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SERIKALI NA MCHANGO WAKE KATIKA USTAWI WA MAHAKAMA, MAENDELEO YA TAIFA NA UPATIKANAJI WA HAKI

Posted on: February 2nd, 2026

Maadhimisho ya Siku ya Sheria Nchini (Law Day) 2026 Kimkoa yamefanyika katika Kiwanja cha Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Buswelu, Wilaya ya Ilemela, yakilenga kuangazia mchango wa Mahakama katika ustawi wa jamii na maendeleo ya Taifa.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema Serikali itaendelea kushirikiana na mhimili wa Mahakama kwa kuwa ni mdau muhimu katika kusimamia haki na kuhakikisha wananchi wanapata haki kwa wakati.

Mhe. Mtanda amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwekeza katika ujenzi wa Mahakama na kuimarisha upatikanaji wa haki kupitia kampeni ya Mama Samia Legal Aid.

Amesema kupitia kampeni hiyo, mashtaka 1,572 yamesikilizwa, kesi 580 zimekamilika huku kesi 992 zikiendelea kufanyiwa kazi, pamoja na kutolewa elimu ya sheria na huduma za utatuzi wa migogoro.

Mhe. Mtanda amesema katika kupunguza mlundikano wa mashauri Mahakamani, Serikali imekuwa ikitatua kero kuanzia ngazi za chini kabla hazijageuzwa kuwa mashauri ya Mahakama.

“Kwa Mkoa wa Mwanza, jumla ya kero 249 zimesikilizwa ambapo 213 zimekamilika na 36 zinaendelea kufanyiwa kazi”.

Kwa upande wake, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mwanza, Mhe. Dkt. Ntemi Kilekamajenga amesema Siku ya Sheria ni fursa ya kujitathmini endapo haki imetendeka na kuonekana kwa wananchi.

Amebainisha kuwa Mahakama ni mlinzi wa Katiba, mlezi wa haki za raia na ngome ya wanyonge, sambamba na kusukuma maendeleo ya Taifa kupitia amani na utulivu.

Amesema kuanzia Januari hadi Desemba 2025, kesi 15,105 zilifunguliwa katika Mahakama za Kanda ya Mwanza, kesi 18,236 zikaamuliwa huku kesi 4,086 zikiendelea.

Naye Wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mkoa wa Mwanza, Bw. Kabyemela S. Lushagara amesema Siku ya Sheria ni kioo cha kutafakari wajibu wa Sheria na Mahakama katika kulinda haki, amani na usawa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MADIWANI MWANZA WAJENGEWA UWEZO UONGOZI NA USIMAMIZI WA MAENDELEO

    February 02, 2026
  • SERIKALI NA MCHANGO WAKE KATIKA USTAWI WA MAHAKAMA, MAENDELEO YA TAIFA NA UPATIKANAJI WA HAKI

    February 02, 2026
  • RMO MWANZA AZINDUA KAMBI YA UPIMAJI AFYA KWA WANANCHI

    January 31, 2026
  • NYANZA YATAKIWA KUHAKIKISHA PEMBEJEO ZA PAMBA ZINAWAFIKIA WAKULIMA KWA WAKATI

    January 30, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.