• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA

Posted on: February 5th, 2026

Serikali kupitia Baraza la Ushindani (FCT) imeendesha semina kwa wadau wa Mkoa wa Mwanza, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ufanisi wa utekelezaji wa sheria za ushindani.

Semina hiyo imefanyika leo Februari 05 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ikujumuisha wadau kutoka sekta mbalimbali za biashara.

Akifungua semina hiyo, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amesema kwamba semina hiyo ni muhimu kwa wadau wa sekta ya biashara kwa kuwa itawawezesha kuelewa vyema majukumu ya Baraza la Ushindani na umuhimu wa kuendeleza mshikamano katika utekelezaji wa sheria za ushindani.

Amesema kuwa, “Kupitia semina hii, tutapata uelewa mpana zaidi wa Baraza la Ushindani na umuhimu wa kulinda haki za mlaji na kuendeleza ushindani wa haki katika soko.”

Baraza la Ushindani (Fair Competition Tribunal – FCT) ni taasisi ya serikali iliyo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara. Lengo lake kuu ni kutatua migogoro ya kiushindani kwa njia ya rufaa kutoka kwa taasisi za udhibiti kama vile Tume ya Ushindani (FCC), EWURA, LATRA, TCAA, na TCRA. Ameongeza Katibu Tawala huyo.

Bw. Elikana ameeleza kuwa semina hiyo itawanufaisha washiriki kwa kuimarisha ufahamu wao kuhusu haki na wajibu wao katika masuala ya ushindani, na hivyo kuongeza uwajibikaji katika utekelezaji wa sheria.

“Serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha ili kuhakikisha soko linakuwa na ushindani wa haki na linamlinda mlaji,” ameongeza.

Wadau wamehamasishwa kutoa maoni na ushauri kuhusu kuboresha mawasiliano kati ya Baraza la Ushindani na wadau wa sekta mbalimbali, ili kufanikisha malengo ya kuongeza ufanisi na uwazi katika soko.

Serikali kupitia Baraza la Ushindani imesema itaendelea kuwa na ushirikiano wa karibu na wadau wote ili kuhakikisha utekelezaji wa majukumu yao unafanikiwa na soko linakuwa na ushindani wa haki.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA

    February 05, 2026
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA

    February 04, 2026
  • KANDA YA ZIWA YAPIGWA MSASA UWEKEZAJI, DIRA YA TAIFA 2050 YATAJWA MSINGI WA MAPINDUZI YA UCHUMI

    February 04, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WAKANDARASI WA UMEME MWANZA KUFANYA KAZI KWA UADILIFU

    February 02, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.